Tafuta

Tetemeko Siria na Uturuki:Mtoto akiondolewa kwenye vifusi vya nyumba baada ya kuporomoka. Tetemeko Siria na Uturuki:Mtoto akiondolewa kwenye vifusi vya nyumba baada ya kuporomoka.  (ANSA)

Uturuki na Siria:tetemeko limeharibu ofisi za Caritas,lakini wahudumu kibinadamu wanatoa msaada

Mkurugenzi wa Caritas Siria,ameelezea kuwa nchini Siria,tetemeko la ardhi liliathiri sana kaskazini-magharibi mwa Siria,eneo ambalo watu milioni 4.1 wanategemea msaada wa kibinadamu.Takriban watu 5,000 waliokimbia makazi yao,wengi wao wakiwa wanawake na watoto, wamepata makazi katika shule na kumbi.

Na Angella Rwezaula; - Vatican.

Tetemeko la ardhi la kipimo cha 7.8 lililotokea kaskazini-magharibi mwa Siria na Uturuki limesababisha maelfu ya watu kukosa makazi, chakula na mafuta. Caritas Uturuki na Caritas Siria walikuwa wakitoa msaada tangu mwanzo na Shirikisho la Caritas Internationalis linaunga mkono na kuratibu juhudi zao za kutathmini mahitaji na kutoa msaada kwa walioathiriwa na janga hili. Maeneo yaliyokumbwa na tetemeko la ardhi tayari yalikuwa katika hali ngumu ya kibinadamu. Baridi kali katika msimu wa baridi na uharibifu au uharibifu mkubwa wa miundo  ikiwa ni pamoja na hospitali kadhaa na wakati huo huo barabara kuzidisha ugumu wa shughuli za kibinadamu.

Kikundi cha watu wa kijitolea  na mbwa maalum wa kusaidia kutoa watu watu waliofunikwa na vifusi  kutoka Italia kuelekea Uturuki
Kikundi cha watu wa kijitolea na mbwa maalum wa kusaidia kutoa watu watu waliofunikwa na vifusi kutoka Italia kuelekea Uturuki

Riad Sargi, Mkurugenzi wa Caritas Siria, ameelezea kuwa nchini Siria, tetemeko la ardhi liliathiri sana kaskazini-magharibi mwa Siria, eneo ambalo watu milioni 4.1 wanategemea msaada wa kibinadamu. Takriban watu 5,000 waliokimbia makazi yao, wengi wao wakiwa wanawake na watoto, ambao wamepata makazi katika shule na kumbi. Idadi ya vifo na majeruhi iliyorekodiwa inaendelea kuongezeka huku msako wa kuwatafuta watu waliopotea miongoni mwa vifusi vya majengo na nyumba zilizoharibiwa ukiendelea. Hospitali katika baadhi ya maeneo yaliyoathirika zaidi zilizidiwa wakati zikifanya kazi ya kuwatibu waliojeruhiwa na tetemeko hilo la ardhi.

Askari wa Uturuki akisikitika mbele ya nyumba zilizoanguka huko Hatay,Uturuki 7 Februari 2023.Maelfu na maefu ni majeruhi na vifo vingi
Askari wa Uturuki akisikitika mbele ya nyumba zilizoanguka huko Hatay,Uturuki 7 Februari 2023.Maelfu na maefu ni majeruhi na vifo vingi

Caritas Siria kwa hiyo inafanya kazi ya kutoa vifaa vya usaidizi na kufungua makazi ili kuwahudumia wale wanaohitaji zaidi huko Aleppo, Hama na Lattakia. Ni baridi sana na inaendelea kuanguka na theluji. Wengi wamepoteza makazi yao na hata wale ambao bado wana nyumba hawarudi kwao kwa kuhofia kushtuka Zaidi,alisisitiza  Sargi. Huko Aleppo, vitu vya msaada na makazi ya watu ambao nyumba zao zilibomoka zinahitajika. Ofisi ya Caritas Aleppo iliharibiwa, pamoja na nyumba nyingi za wafanyakazi. Nchini Uturuki, mikoa ya kusini-mashariki ya nchi hiyo ikiwa ni pamoja na Kahramanmaraş, Hatay, Osmaniye, Adıyaman, Gaziantep, Şanlıurfa, Diyarbakır, Malatya na Adana iliathiriwa na tetemeko la ardhi na mitetemeko midogo mfululizo 42, baada ya tetemeko, kubwa zaidi ikiwa na la ukubwa wa 6.6.

Tarehe 6 Februari wakati nyumba zikiangushwa na tetemeko
Tarehe 6 Februari wakati nyumba zikiangushwa na tetemeko

Jimbo la mkoa wa Anatolia limeathiriwa sana na tetemeko la ardhi na Kanisa kuu la Iskenderun lilianguka kabisa. Ofisi za Caritas Anatolia ziliharibiwa vibaya. Lakini “Nashukuru Mungu wafanyakazi wako salama, lakini tumepoteza watu wa kujitolea, wafadhili na hata ndugu” alisema, Giulia Longo, Meneja Programu wa Caritas Uturuki, ambaye alikuwa Italia wakati wa tetemeko la ardhi pamoja na rais wa shirika hilo, Monsinyo Paolo Bizzeti, na sasa amerejea Uturuki. Kwa upande wake alisema “Rais na mimi tuko hai kwa muujiza. Kama tungekuwa Iskenderun pengine tusingeokolewa,” Longo alisema.

Wakati wa operesheni mtoto wa miaka 8 hivi ameokoòlewa kutoka kwenye vifusi kwa masaa40  baada ya tetemeko huko Salqin kaskazini mwa Siria
Wakati wa operesheni mtoto wa miaka 8 hivi ameokoòlewa kutoka kwenye vifusi kwa masaa40 baada ya tetemeko huko Salqin kaskazini mwa Siria

Caritas Uturuki mara moja ilifungua simu ya dharura ya Kituo cha Kusikiliza ili kutoa msaada na usaidizi kwa wale walioathiriwa na maafa, na kwa sasa inafanya kazi pamoja na mamlaka mahalia katika kukusanya taarifa na kuandaa jibu la kibinadamu. Kwa kuongezea, timu za Caritas zimekuwa zikiwakusanya watu waliohamishwa katika maeneo salama na ya wazi na kujaribu kusambaza chakula cha moto na nguo. Shirikisho la Caritas linaunganisha juhudi zao na kufanya kazi kwa pamoja ili kutoa misaada ya kibinadamu kwa wale wanaohitaji zaidi na kuomba msaada na maombi endelevu ya jumuiya ya kimataifa katika kupunguza mateso ya watu nchini Siria na Uturuki kwa wakati huu.

08 February 2023, 13:46