Vatican ina wasi wasi wa kukamatwa Kardinali Zen huko Hong Kong
Na Angella Rwezaula – Vatican.
Kardinali Joseph Zen, mwenye umri wa miaka 90, aliyekuwa Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki la Jimbo Hong Kongo kuanzia mwaka 2002 hadi 2009, alikuwa amekamatwa na Polisi, Jumatano 11 Mei 2022. Kardinali huyo ameachiliwa kwa dhamana tarehe hiyo hiyo 11 Mei 2022, majira ya saa 11 jioni kwa saa za Italia, kama ilivyotangazwa na waandishi wa habari wa Hong Kong ambao pia walichapisha picha za Kardinali Zen akiwa nje ya kituo cha polisi cha Wan Chai kwenye mitandao ya kijamii. Alipotoka, Kadinali aliingia mara moja kwenye gari la kibinafsi lililokuwa limeegeshwa karibu, bila kutoa maoni yoyote. Alisindikizwa na watu watano. Kutokana na hilo Vatican imeelezea wasiwasi wake baada ya kupata habari za kukamatwa kwa Kardinali Zen na inafuatilia hali halisi kwa umakini mkubwa. Alisema hayo alasiri Msemaji mkuu wa Vyombo vya Habari vya Vatican, Dk. Matteo Bruni, akijibu maswali ya waandishi wa habari.
Kukamatwa na kufunguliwa mashtaka
Kardinali Zen alikuwa amesimamishwa Jumatano na kitengo cha polisi kilichoundwa ili kuangalia usalama wa taifa la China na baadaye alihojiwa katika kituo cha polisi cha Wan Chai. Shutuma dhidi ya kadinali huyo wanabainisha kwamba ni ya kula njama na majeshi ya kigeni" kuhusiana na jukumu lake kama msimamizi wa Hazina ya Misaada ya Kibinadamu ya 612, mfuko ambao uliunga mkono waandamanaji wanaounga mkono demokrasia katika kulipa gharama za kisheria au afya walizopaswa kukabiliana nazo.
Wafungwa wengine watatu
Kadinali ni mtawa wa Kisalesian alikuwa mmoja wa wadhamini wa shirika hilo, lililoanzishwa mnamo 2019 na kufutwa mwezi Oktoba mwaka jana. Mbali na Kardinali Zen, mamlaka pia iliwakamata waendelezaji wengine wa Hazina, akiwemo mwanasheria maarufu Margaret Ng, mbunge wa zamani wa upinzani, mwanataaluma Hui Po-keung na mwimbaji na mtunzi wa nyimbo Denise Ho. Kukamatwa kwao kulithibitishwa na vyanzo vya kisheria vya Hong Kong. Kulingana na wanahabari wa Hong Kong, wao pia waliachiliwa kwa dhamana.
Uchunguzi
Vyombo vya habari vya ndani viliripoti kwamba uchunguzi wa polisi, ambao ulianza mwezi Septemba iliyopita, ulizingatia madai ya Kula njama ya Mfuko wa 612 na vikosi vya kigeni, kinyume na sheria ya usalama wa kitaifa iliyowekwa na Beijing mnamo Juni 2020. Ni moja ya makosa manne yaliyotazamiwa na Sheria ya Usalama wa Kitaifa na iliyolaaniwa kimataifa, kuzima maandamano ya demokrasia katika koloni hilo la kizamani. Makosa mengine ni uasi, kujitenga na ugaidi na inaweza kusababisha hukumu ya kifungo cha je ya maisha. Katika miezi ya hivi karibuni, baadhi ya magazeti ya Hong Kong yalimshutumu askofu huyo aliyeibuka kwa kuwachochea wanafunzi kuasi dhidi ya mfululizo wa hatua za serikali mwaka 2019. Katika siku za nyuma, Zen pia alikuwa mstari wa mbele kwa kukosoa Chama cha Kikomunisti cha China kwa kukemea shinikizo na mateso kwa jumuiya za kidini.
.