Kimbunga Gezani nchini Madagascar kilisababisha madhara makubwa. Kimbunga Gezani nchini Madagascar kilisababisha madhara makubwa. 

Madagascar:Majimbo ya nchi yajipanga kusaidia familia zilizokumbwa na kimbunga

Majimbo yote katoliki nchini Madagascar yamejipanga kusaidia familia zilizoathiriwa na Kimbunga Gezani.Hayo yalisemwa na Askofu Rosario Vella,SDB, akizungumza na Shirika la Kipapa la Habari za Kimisionari Fides kuhusu kimbunga Gezani kilichopigisha magoti kisiwa kikubwa."Ilikuwa wakati mgumu sana kwa watu,na pia kwa jumuiya nzima ya Kikristo,kwani makanisa mengi pia yalipata uharibifu mkubwa.Kanisa huko Tamatave lilibomolewa.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Askofu wa Moramanga, Rosario Vella, SDB, alipokuwa jijini Roma, alizungumza na Shirika la Kipapa la Habari za Kimisionari Fides kuhusu matokeo ya Kimbunga cha Kitropiki Gezani, ambacho kilipiga kisiwa cha Madagascar hivi karibuni. Katika maoni yake Askofu huyo alisema kuwa "Ilikuwa wakati mgumu sana kwa watu, na pia kwa jumuiya nzima ya Kikristo, kwani makanisa mengi pia yalipata uharibifu mkubwa. Kanisa huko Tamatave lilibomolewa kabisa na paa likaharibiwa." Madagascar inakabiliwa na vimbunga kila mwaka, na mwaka huu Gezani ilisababisha uharibifu mkubwa sana katika sehemu ya kati ya nchi, kuanzia moja kwa moja katika jiji la Tamatave.

Watu hawana mahali pa kulala
Watu hawana mahali pa kulala   (AFP or licensors)

Kimbunga hicho kiliibuka katika Pasifiki na kugonga jiji kwa nguvu kubwa sana, na kusababisha mvua na upepo wa kilomita 240-245 kwa saa, na kuharibu vibaya kati ya 75% na 80% ya nyumba. "Sehemu zote za pembezoni, au tuseme, maskini, za jiji, ambapo nyumba hazitengenezwi kwa matofali na kwa kiasi kikubwa ni vibanda vya mbao au majani, zilisombwa kabisa. Sote tulichukua hatua mara moja, si kwa ajili ya nyumba tu,  bali pia na hasa kwa familia zilizopoteza karibu kila kitu walichokuwa nacho.”

Uzinduzi wa usaidizi kutoka majimbo yote ya nchi

Katika majimbo yote, kupitia mashirika mbalimbali ya kijimbo na kitaifa ya Caritas, makusanyo yamezinduliwa kwa ajili ya kukusanya pesa, chakula, mavazi, na nyenzo nyingine yoyote muhimu kwa maisha ya kila siku. Hata jimbo, ambalo kwa kawaida hufanya kidogo sana katika visa hivi, linaonekana kuimarika wakati huu, na tunatumai ushirikiano huu utatoa matokeo mengi chanya.

Maji yaliyojaa kila kona
Maji yaliyojaa kila kona   (AFP or licensors)

“Jimbo langu linapakana na eneo lililoathiriwa, lakini, namshukuru Mungu, ikiwa umbali wa takriban kilomita 200, haikuathiriwa sana. Baadhi ya makanisa yalikuwa yameezekwa paa, mengine yamebomoka." Katika jumuiya ya watawa, shule pia iliharibiwa vibaya, na baadhi ya majengo yaliharibiwa kabisa. Kurudi kwake Jimboni Askofu wa Moramanga tayari alipanga kutembelea maeneo yaliyoathiriwa mara moja, kwa huruma kwa waathiriwa na kutathmini kiwango cha uharibifu.

MADAGASCAR KIMBUNGA OK

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku. Just click here

20 Februari 2026, 14:23