2026.04.03 Nigeria: Askofu  Matthew Hassan Kukah wa Jimbo Sokoto 2026.04.03 Nigeria: Askofu Matthew Hassan Kukah wa Jimbo Sokoto 

Jimbo la Sokoto,Nigeria,lakataa madai ya kushambuliwa kwa Kanisa Kuu

Kujibu ripoti za uongo za kushambuliwa kwa makazi ya Askofu,Kanisa kuu,na kituo cha wachungaji,Jimbo la Sokoto linatoa kanusho rasmi linalokataa madai hayo.

Vatican News

Jimbo Katoliki la Sokoto, Nigeria, limechapisha kanusho rasmi linalokataa madai kwamba makazi ya Askofu, Kanisa kuu na kituo cha wachungaji cha Jimbo vilishambuliwa. Taarifa hiyo, iliyosainiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano, Padre Pascal Salifu, iliyoelezea video ya habari za uongo ambayo ilisambaa sana. Taarifa ya Jimbo  ilifafanua kwamba vifaa vyote viko salama, havina madhara, na vinafanya kazi kikamilifu na kwamba madai haya ni ya uwongo kabisa.

Kanisa Katoliki nchini Nigeria limesisitiza mara kwa mara jinsi taarifa potofu zinavyotumika kugawanya nchi. Kwa hivyo, wito ni kuthibitisha habari kila wakati ili kutosambaza habari bandia ambazo zinaweza kusababisha hasira na vurugu zisizo na ubaguzi. Ufafanuzi wa habari bandia ulifuata badala yake habari ya kweli kutoka  Dominika ya Matawi  iliyopita ya Matawi wakati kulipokuwa na shambulio huko Jos, mji ulio mbali na Sokoto, ambapo watu 27 waliuawa.

Mahojiano na Vatican News

Katika mahojiano na Vatican News iliyochapishwa tarehe 4 Aprili 2026, Askofu wa Sokoto, Matthew Hassan Kukah, alielezea umuhimu wa kudumisha mtazamo wa matumaini katikati ya vurugu zinazoendelea nchini. Wakati huo huo alilaani mashambulizi hayo na kuwahimiza watu “wasikubali kuogopa bali badala yake wamtegemee Mungu na kubaki imara.”

JIMBO LA SOKOTO

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata taarifa mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku:Just click here.

08 Aprili 2026, 11:49