2025.11.24 Papa alikutana na Bi Evika Silina, Waziri Mkuu wa Latvia. 2025.11.24 Papa alikutana na Bi Evika Silina, Waziri Mkuu wa Latvia.  (@VATICAN MEDIA)

Papa akutana na Waziri Mkuu wa Latvia

Kwa mujibu wa taarifa za Ofisi ya Vyombo vya Habari Vatican, imebainisha kuwa tarehe 24 Novemba 2025,Papa Leo alikutana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Latvia, Mheshimiwa Bi Evika Siliņa,ambaye baadaye alikutana na Kardinali Parolin,Katibu Mkuu wa Vatican,akifuatana na Askofu Mkuu Gallagher,Katibu wa Vatican wa Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa.

Vatican News.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyombo vya Habari, Vatican imebanisha kuwa “Asubuhi ya leo, tarehe 24 Novemba 2025, Baba Mtakatifu  Leo XIV alimpokea kwa Mkutano  katika Jumba la  Kitume la Vatican, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Latvia, Mheshimiwa  Bi Evika Siliņa, ambaye baadaye alikutana na Kardinali Pietro Parolin, Katibu Mkuu wa Vatican , akifuatana na Askofu Mkuu Paul R. Gallagher, Katibu wa Vatican wa  Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa.”

Mkutano wa waziri Mkuu wa Latvia na Papa
Mkutano wa waziri Mkuu wa Latvia na Papa   (@VATICAN MEDIA)

Wakati wa mazungumzo ya kirafiki katika Sekretarieti ya Vatican, pande zote mbili zilielezea kuridhika na uhusiano mzuri kati ya Vatican na Jamhuri ya Latvia, pamoja na mchango chanya ambao imani ya Kikristo na Kanisa Katoliki hutoa kwa nchi. Mazungumzo hayo pia yaligusia masuala kadhaa ya kikanda na kimataifa, hasa juhudi za kufikia amani na kukomesha vita nchini Ukraine.

Waziri Mkuu wa Latvia akizungumza na Katibu Mkuu wa Vatican
Waziri Mkuu wa Latvia akizungumza na Katibu Mkuu wa Vatican   (@Vatican Media)
Waziri Mkuu wa Latvia
24 Novemba 2025, 12:28