Kimbuga kikali nchini Uphilippino Kimbuga kikali nchini Uphilippino  (AFP or licensors)

Papa Leo XIV ameonesha ukaribu kwa waathirika wa kimbunga huko Ufilipino

Papa yuko karibu na waathiriwa wa kimbunga kikali Ufilipino.Na pia alitoa shukrani zake za dhati kwa wale katika kila ngazi wanaofanya kazi ya kujenga amani katika maeneo mbalimbali yaliyoathiriwa na vita.Katika siku za hivi karibuni amesema“tumewaombea marehemu,na kwa kusikitisha,miongoni mwao wengi wameuawa katika mapigano na mabomu ingawa walikuwa raia,watoto,wazee,na wagonjwa.Ikiwa kweli tunataka kuheshimu kumbukumbu zao,tusitishe mapiganona tuwe na mazungumzo.”

Na Angella Rwezaula – Vatican

Mara baada ya Tafakari na sala ya Malaika wa Bwana, Dominika tarehe 9 Novemba 2025, Baba Mtakatifu leo VI ameonesha ukaribu na watu wa Ufilipino waliokumbwa na kimbuka kikali. Papa amesema “Niko karibu na watu wa Ufilipino walioathiriwa na kimbunga kikubwa: Ninawaombea marehemu na familia zao, waliojeruhiwa na waliokimbia makazi yao.”

Kimbunga kikali nchini Ufilipino:mlundikano wa watu
Kimbunga kikali nchini Ufilipino:mlundikano wa watu

Nchini Italia ikiwa ni siku ya kutoa shukrani kwa mwenyezi  Mungu Papa Leo XIV alisema  kuwa “ Leo Kanisa nchini Italia linaadhimisha Siku ya Shukrani. Ninajiunga na ujumbe wa Maaskofu katika kuhimiza utunzaji wa ardhi kwa uwajibikaji, mapambano dhidi ya upotevu wa chakula, na kupitishwa kwa mbinu endelevu za kilimo. Tumshukuru Mungu kwa "dada yetu mama dunia" (Mtakatifu Francisko wimbo wa sifa kwa viumbe) na kwa wote wanaolima na kuilinda!”

Salamu mbali mbali kwa moyo wote kwanza kabisa Warumi, na mahujaji kutoka pande za Italia na sehemu nyingi za dunia, kwa namna ya pekee vijana Wajesuit kutoka Poland, waamini waliotoka Warsaw na Danzica, Poland, Newark na Carney nchini Marekani,  Toledo, ya Galapagar huku Hispania na London  na kama ilivyo Kwaya ya  Regensburger Domspatzen.

Papa aliendelea kusema kuwa “Salamu kwa Chama cha matendo ya Kitume Katoliki Jimbo Kuu la Genova, na Makundi ya Parokia ya Cava Manara, Mede, Vibomarina, Mtakatifu Malaka Mkuu huko Potenza, Noto, Pozzallo na Avola, Cesenatico, Mercato Mtakatifu Severino, Crespano ya Grappa na Noventa Padovana.” Aidha “Salamu kwa Kundi la maandamano ya kihistoria ya Lazio na watu wa kujitolea wa Meza vya vyakua ambao watakusanya vyakula Jumamos ijayo katika keshoa la Siku ya Maskini Ulimwenguni.”

Wanaoomboleza kufuatia na vifo vya ndugu zao wasio na hatia
Wanaoomboleza kufuatia na vifo vya ndugu zao wasio na hatia   (AFP or licensors)

Papa Leo XIV kadhalika alitoa shukrani zangu za dhati kwa wale katika kila ngazi wanaofanya kazi ya kujenga amani katika maeneo mbalimbali yaliyoathiriwa na vita. Katika siku za hivi karibuni tumewaombea marehemu, na kwa kusikitisha, miongoni mwao wengi wameuawa katika mapigano na mabomu, ingawa walikuwa raia, watoto, wazee, na wagonjwa. Ikiwa kweli tunataka kuheshimu kumbukumbu zao, hebu tusitishe mapigano na tujitoe kwenye mazungumzo.

Nawatakia kila mmmoja Dominika njema!

Baada ya Angelus

Asante kwa kusoma makala haya. Ikiwa ungependa kuendelea kupata taarifa mpya, tafadhali jiandikishe kwa jarida letu kwa kubofya hapa: cliccando qui

 

09 Novemba 2025, 15:03