2025.11.30 Ziara ya Kitume  Libanon:Papa atembelea Monasteri ya Wakarmeli wa Mama wa Mungu. 2025.11.30 Ziara ya Kitume Libanon:Papa atembelea Monasteri ya Wakarmeli wa Mama wa Mungu.  (@Vatican Media)

Papa Leo XIV awatembelea Watawa Wakarmeli huko Harissa,Lebanon

Kwa dakika 30,Papa Leo XIV aliwatembelea Masista Wakarmeli wa Theotokos yaani wa Mama wa Mungu huko Harissa,jioni ya Dominika Novemba 30,katika siku yake ya kwanza akiwa huko Lebanon.

Vatican News

Mara baada ya kukutana na mamlaka,  mamlaka ya kiraia, wawakilishi wa asasi za kiraia, na kikundi cha kidiplomasia cha Jamhuri ya Lebanon, Dominika  jioni, tarehe 30 Novemba 2025, Baba Mtakatifu Leo XIV alisafiri hadi kwenye Monasteri ya Masista Wakarmeli wa Theotokos yaani wa Mama wa Mungu, huko Harissa. Kulingana na taarifa kutoka Ofisi ya Habari ya  Vatican ilibanisha kuwa, "Papa aliwasalimia kila sista  mmoja mmoja kabla ya kupokea salamu kutoka kwa wakuu wa jumuiya hizo mbili.

Wakuu wa jumuiya mbili za watawa wakarmeli mbele ya Papa wakimpatia zawadi
Wakuu wa jumuiya mbili za watawa wakarmeli mbele ya Papa wakimpatia zawadi   (@Vatican Media)

Akiwahutubia watawa hao "Papa Leo XIV  aliwakumbusha maneno matatu katika kiini cha wito wao wa kutafakari ambayo ni: unyenyekevu, sala na sadaka."

Papa akisaini kitabu chao cha wageni
Papa akisaini kitabu chao cha wageni   (@Vatican Media)

kwa mujibu wa taarifa ni kwamba "Mkutano huo ulidumu kwa takriban nusu saa na kuhitimishwa kwa kusali sala ya Baba Yetu, na Papa Leo XIV aliwapatia Baraka yake ya Kitume watawa Wakarmeli wa ndani.

Papa akiwahutubia watawa hao
Papa akiwahutubia watawa hao   (@Vatican Media)
Watawa wakipiga makofi
Watawa wakipiga makofi   (@Vatican Media)
Papa akimsalimia mmoja baada ya mwingine
Papa akimsalimia mmoja baada ya mwingine   (@Vatican Media)
Papa akionesha picha
Papa akionesha picha   (@Vatican Media)

Pope Leo poses for a group photo with the nuns

Hatimaye picha ya pamoja na Papa na watawa wakarmeli (@Vatican Media).

 

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku: Just click here

30 Novemba 2025, 21:18