Baada ya Ziara ya Papa barani Afrika, anatarajia kwenda Ufaransa. Baada ya Ziara ya Papa barani Afrika, anatarajia kwenda Ufaransa.  (ANSA)

Ziara ya Papa Leo XIV kwenda Ufaransa 25-28 Septemba 2026

Kwa kukaribishwa na Mkuu wa Nchi na Mamlaka ya Kikanisa cha Nchi na ile ya Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO,Baba Mtakatifu Leo XIV atatimiza Ziara ya Kitume nchini Ufaransa kuanzia tarehe 25 hadi 28 Septemba 2026 na kutembelea makao makuu ya Shirika.

Vatican News

Baada ya Hispania, Ziara ya Kitume ya Papa Leo XIV itakayofuata  itakuwa tena katika nchi ya Ulaya, huko Ufaransa.

Ofisi ya Habari ya Vatican  Jumamosi tarehe 16 Mei 2026 ilitangaza kuwa: "Kwa kukubali mwaliko wa mkuu wa nchi na mamlaka ya kikanisa ya nchi hiyo, na ule wa Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO, Baba Mtakatifu Leo XIV atafanya ziara yake ya  kitume kwenda Ufaransa kuanzia tarehe 25 hadi 28 Septemba 2026, na atatembelea makao makuu ya Shirika hilo," taarifa ilisomeka.

Hii itakuwa Ziara ya  tano ya Kimataifa ya Papa Leo XIV, kufuatia  na zile za Uturuki na Lebanon (Novemba 27 - Desemba 2, 2025), Ufalme wa  Monaco (Machi 28), Afrika (Aprili 13 - 23), na Hispania  itakayofanyika kuanzia (Juni 6 - 12).

Ziara ya Papa Ufaransa

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here.

16 Mei 2026, 13:19