Jalida la ‘Piazza San Pietro:"Udugu katika likizo,tusiwaache wazee peke yao"
Vatican.
Baba Mtakatifu Leo XIV katika kujibu swali aliloulizwa kwenye jalida la kila mwezi liitwalo: “Piazza San Pietro”kwa swali: “Mpendwa Papa jinsi gani ya kuboresha imani katika likizo? Papa anajibu kwa kina akitafakari juu ya wale ambao kwa hakika hawawezi kwenda likizo kutokana na miktadha tofauti ya maisha. Ifuatao ni barua ya jibu la Baba Mtakatifu kwa mwandishi:
Barua kamili ya Papa Leo XIV kwa Maurizio
Mpendwa Maurizio, asante kwa barua yako ambayo inaniruhusu kufanya tafakari kuhusu likizo ambayo inakaribia. Zingatio la kwanza linahusu maskini na wale wote ambao hawawezi hata kuishi kipindi kifupi cha likizo, kwa sababu wamekandamizwa na uzito wa matatizo ya kila aina. Hakuna matatizo ya uchumi tu, ambayo yanazuia watu kuishi, na angalau hata kwa siku chache, katika utulivu na katika amani ya moyo. Tuwafikirie wagonjwa, watu ambao wamepoteza imani katika maisha, mtu ambaye amekumbwa na uchungu kwa sababu ya kupoteza wapendwa binafsi, wahanga wa vita, wa chuki, wa ugaidi na wa vurugu, wanaoteswa kwa sababu ya imani na ya haki, kwa wafungwa, na ambaye amebaki bila kazi, bila nyumba, wahamiaji ambao hawapokelewi kibinadamu. Likizo inapaswa iwe kwa wote hata nafasi moja ya kuacha shughuli na wasiwasi, ili kuweza kuishi uzoefu wa dhati wa urafiki, wa kushirikishana, kwa namna ya kufanya, kwanza uzoefu wa udugu na ushirika ambao tunaweza kuishi na tutaishi katika Ufalme wa Mungu. Kwa namna pekee kwa wakristo, familia, wazazi kama ilivyo kwa watoto, vijana na kwa wazee zaidi, ninawatakia kwamba, likizo ya kiangazi iwe fursa kwa ajili ya matunda ya uzoefu wa kijamii na kidini, kwa ajili ya kutafakari kwa kina utume wa Kanisa na katika jamii.
Ni matumaini zaidi kwamba wakati wa kipindi cha miezi hii ya kiangazi wagonjwa wasikose ukaribu wa familia zao, watu wa kujitolea na watu ambao wanaweza kuamua sehemu ya likizo kupita jitihada ya kidugu na kijamii. Kwa familia, ninawaeleza: msiwaache wazee wenu peke yao. Na kwa watu wa kujitolea, vijana na watu wazima: jitihadini kupeleka ubinadamu na matumaini kwa wanaoteseka na mtano matunda ya neema, mtaona jinsi gani upendo utawajia katika maisha yenu, na jinsi gani mnajazwa furaha. Tazama huu ndiyo ushauri ambao ninaweza kuwapatia ili kukua katika imani yetu. Kuutumia hata wakati wa kiangazi ili kuishi Injili ya amani na ya huruma.
Tuwaze faida ambayo tunaipata tunaposaidia maskini na tunashuhudia umaskini wa kiinjili. Hii ni huduma ambayo tunamfanyia Kristo mwenyewe. Na kwa hiyo wakati wa likizo, tuepuke hata matumizi yasiyo na tija, mambo mengi na kutumia hovyo, bali tujielimishe kiasi. Tukumbuke daima kwamba, kuwa na mali nyingi: kunazuia uinjilishaji. Hata likizo ziendane na mtindo wa maisha. Upendo na neema ya Mungu vinatufikia kila siku na daima. Tusaidiane, kila jumuiya, na tusipoteze urithi huo wa ubinadamu na amani, ambalo ni tumaini pekee la kutoa mstakabali wa ulimwengu unaotishiwa na vita. Hakuna nguvu za dunia hii, zitakazookoa Ulimwengu, kama nilivyokuwa nimesema katika Madhabahu ya Mama wa Pompei, mnamo tarehe 8 Mei iliyopita, bali ni nguvu ya kimungu tu ya upendo ambao Yesu, Bwana alituonesha na kujitoa. Tuamini kwake, tuamini Yeye, na tumfuate! Ninakushukuru kwa maneno yako Maurizio na Ninakusindikiza na baraka yangu.
Leo PP XIV.
Papa anahitimishwa kwa sahihi yake hiyo.
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here.
