Papa Leo XIV kwa Vijana wa Czech:Shuhudia Upendo wa Kristo katika Familia&katika Jamii
Vatican News
Baba Mtakatifu Leo XIV ametoa mwaliko kwa washiriki katika Mkutano wa Kitaifa wa Vijana, ulioanza, Agosti 11, huko Ostrava, Jamhuri ya Czech, na unaendelea hadi Dominika tarehe 16 Agosti 2026. Katika ujumbe huo Papa anawasihi wawe "Karibu kwa bidii uwepo hai wa Kristo na nuru ya neno lake, ili kuwa mashuhuda wa upendo wake katika familia, katika jamii, na katika mazingira mbalimbali ya maisha, kazi, na masomo." Hawa ni zaidi ya vijana elfu tatu wa kiume na kike wenye umri wa miaka kuanzia 14 hadi 26 wanashiriki.
![]()
Vijana washiriki wa Mkutano wa Kitaifa wa vijana huko Ostrava (© CSM Ostrava 2026).
Sala na kutia Moyo
Katika ujumbe uliosainiwa na Katibu Mkuu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin, ulioelekezwa kwa Askofu Mkuu Josef Nuzík, Rais wa Baraza la Maaskofu wa Czech, Papa anatuma "salamu zake za upendo" kwa washiriki wote na "anawatia moyo kumgeukia Bwana Yesu kwa imani, ambaye ameshinda ulimwengu."
Katika maandishi yanasomeka, "Mwokozi, anaendelea kuongoza njia ya wanafunzi wake wote, akiwapatia tumaini, furaha, na amani mioyoni mwao, kwa hivyo, mwaliko kwa vijana ni "kuwa mashuhuda wa upendo wa Mungu katika kila nyanja ya maisha na jamii." Kwa wote, Papa Leo XIV anawahakikishia "ukumbusho wa Baba katika sala" na anatuma baraka zake za kitume, akitamani "tukio hilo liwe na matokeo mazuri, fursa ya kuzaliwa kwa urafiki mpya na wa kweli katika Bwana."
![]()
Washiriki wa Mkutano wa Kitaifa wa Vijana wa Ostrava (© CSM Ostrava 2026).
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata taarifa mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku. Just click here.
