Papa Paulo VI Papa Paulo VI 

"Octogesima adveniens,"maneno hayo kuhusu utambuzi wa wanawake

Mnamo Mei 14, 1971,Papa Paulo VI alichapisha barua ya kitume kusherehekea kumbukumbu ya miaka themanini ya Rerum Novarum ya Papa Leo XIII,ambayo ilizungumzia haki za wanawake.Kurasa hizo zilizungumzia njaa ya dunia,aina mpya za umaskini,kukataliwa kwa itikadi,ulinzi wa mazingira,na uhuru wa Wakatoliki katika siasa.

Andrea Tornielli

Miaka hamsini na mitano iliyopita, mnamo tarehe 14 Mei  1971, Papa Paulo VI alichapisha waraka Octogesima adveniens, kwa kilatini maana yake “kumbukizi ya miaka themanini” katika kusherehekea kumbukumbu ya miaka themanini tangu kuchapishwa kwa waraka wa Kitume  wa kijamii wa Papa Leo XIII, Rerum novarum, yaani “mambo mapya.” Papa Montini aliandikia akielekeza kwa Kardinali Maurice Roy, Askofu Mkuu wa Quebec na alikuwa Rais wa Baraza la Kipapa la Haki na Amani. Barua hiyo, inayozungumzia umaskini, maendeleo, na kujitolea kisiasa, inapaswa kusomwa baada ya  Populorum progressio, yaani “Maendeleo ya Watu.”

Papa anazungumzia "tofauti dhahiri zilizopo katika maendeleo ya kiuchumi, kiutamaduni, na kisiasa ya mataifa: Pamoja na maeneo yenye viwanda vingi, mengine bado yako katika hatua ya kilimo; pamoja na nchi zinazopitia ustawi, mengine yanapambana na njaa,” na hali tofauti ambazo Wakristo wanajikuta wakiishi: “Katika baadhi ya nchi, wamenyamazishwa, wameshikiliwa kwa tuhuma, na, kwa kusema, wametengwa na jamii, wamefungiwa bila uhuru ndani ya mfumo wa kidikteta. Kwingineko, wanawakilisha kundi la wachache dhaifu, ambalo sauti yao haisikiki vizuri. Katika mataifa mengine, ambapo Kanisa linafurahia hadhi inayotambulika, wakati mwingine rasmi, lenyewe linajikuta linakabiliwa na athari za mgogoro unaotikisa jamii, na baadhi ya wajumbe  wake wanajaribiwa na suluhisho kali na za vurugu, kwa imani kwamba wanaweza kutumaini matokeo ya furaha zaidi.

Ingawa baadhi, bila kujua dhuluma zilizopo, wanajitahidi kurefusha hali iliyopo, wengine wanajiruhusu kushawishiwa na itikadi za mapinduzi zinazoahidi, bila udanganyifu, ulimwengu bora zaidi. Papa Paulo VI aliamuru kwamba mbinu za hatua, kujitolea, na uingiliaji kati halisi ziachwe kwa hukumu ya hali halisi ya mahalia: "Ni jukumu la jumuiya za Kikristo kuchambua hali katika nchi yao kwa uwazi, kuifafanua kwa kuzingatia maneno yasiyobadilika ya Injili, kuchora kanuni za kutafakari, vigezo vya hukumu, na miongozo ya hatua kutoka mafundisho ya Kanisa ya  kijamii."

Baba Mtakatifu alielekeza umakini kwenye jambo lenye umuhimu mkubwa linaloainisha nchi zilizoendelea na zinazoendelea: ukuaji wa miji na kuhama kutoka maeneo ya vijijini hadi miji mikuu. "Katika ukuaji huu usio na utaratibu, wafanyakazi wapya huzaliwa. [...] Badala ya kuhamasisha makutano ya kidugu na kusaidiana, jiji linakuza ubaguzi na hata kutojali; linachochea aina mpya za unyonyaji na utawala, ambapo baadhi, wakikisia mahitaji ya wengine, hupata faida isiyokubalika. Nyuma ya sura za mbele, kuna aina nyingi za umaskini, ambazo hazijulikani hata kwa wale walio karibu nasi; zingine zinaoneshwa ambapo utu wa binadamu unasikitishwa: uhalifu, ujambazi, dawa za kulevya, na unyanyasaji wa kijinsia."

Papa Montini, ambaye kama Askofu Mkuu alikuwa amebainisha matatizo ya mitaa mipya ya Milano wakati wa miaka ya ukuaji wa uchumi, na kama Mrithi wa Petro alifuatilia kwa karibu maendeleo yale ya Roma kwa usaidizi halisi, aliandika: "Ni dharura kujenga upya, kwa ukubwa wa barabara, ujirani, au eneo kubwa la mijini, mfumo wa kijamii ambao mwanadamu anaweza kukidhi mahitaji ya utu wake. Vituo vya maslahi na utamaduni lazima viundwe au kuendelezwa katika ngazi za Jumuiya na za Parokia."

Kifungu katika barua hiyo kimetengwa kwa ajili ya wanawake. Papa, ambaye mwaka uliokuwa umetangulia alikuwa amewatangaza wanawake wawili kuwa Walimu  wa Kanisa: Mtakatifu Teresa wa Avila na Mtakatifu Catherine wa Siena, alitoa wito wa kukomeshwa kwa ubaguzi na sheria zitekelezwe, "kwa maana ya kulinda wito unaofaa kwa wanawake wenyewe na, wakati huo huo, kutambua uhuru wao kama watu binafsi, na haki zao sawa kuhusu kushiriki katika maisha ya kiutamaduni, kiuchumi, kijamii, na kisiasa."

Akirejea kuhusu ukuaji wa idadi ya watu katika nchi maskini, Papa Montini aliita "kusumbua" hiyo "aina ya imani ya hatima, ambayo hata huwakamata wale waliohusika" na "wakati mwingine husababisha suluhisho za aina za imani zilizoinuliwa na propaganda hai kwa ajili ya uzazi wa mpango na utoaji mimba." Papa Paulo VI pia alisisitiza ulinzi wa mazingira, akionya kwamba "kupitia unyonyaji wa asili bila kujali," mwanadamu "anahatarisha kuiharibu na kuwa mwathirika wa uharibifu huo."

Octogesima adveniens ina miongozo muhimu kwa ajili ya kujitolea kijamii na kisiasa kwa Wakristo. "Mkristo anayetaka kuishi imani yake kupitia hatua za kisiasa zinazoeleweka kama huduma hawezi, bila kujipinga, kutoa msaada wake kwa mifumo ya kiitikadi ambayo inapingana kabisa au kimsingi na imani yake na dhana yake kuhusu mwanadamu: wala kwa itikadi ya Marxist, kwa vitu vyake vya kutokuamini Mungu, kwa uchochezi wake wa vurugu na jinsi anavyochukua tena uhuru wa mtu binafsi ndani ya pamoja, huku akikataa kuzidi kwa mwanadamu na historia yake, ya kibinafsi na ya pamoja; wala itikadi ya kiliberali inayodai kuinua uhuru wa mtu binafsi kwa kuuondoa kwenye mipaka yote, ikiuchochea kwa kutafuta maslahi na madaraka pekee.”

Kwa hiyo, Papa Paulo VI anawaonya Wakristo wote pande zote mbili “wanaovutiwa na ujamaa,” ambao “huelekea kuufanya kuwa wakamilifu kwa maneno ya jumla”; na wale wanaofuata itikadi ya kiliberali, akiwaomba wasifanye kuwa wakamilifu wa kifalsafa wa uhuru (leo tungeuita neoliberalism) na bila kusahau kwamba “ni uthibitisho potofu wa uhuru wa mtu binafsi katika shughuli zake, katika motisha zake, katika utekelezaji wa uhuru wake.”

Marejeo ya hitaji la mabadiliko ya ndani ni muhimu, kwa sababu mabadiliko ya kimuundo pekee hayatoshi kuhakikisha jamii yenye haki na utu zaidi. “Leo, watu wanatamani kujikomboa kutokana na uhitaji na utegemezi. Lakini ukombozi huu huanza na uhuru wa ndani ambao lazima uupate tena mbele ya mali na mamlaka yao; Hawatafanikiwa kamwe isipokuwa kupitia upendo unaozidi ubinadamu, na, kwa hivyo, kupitia nia madhubuti ya kutumikia. Vinginevyo, kama ilivyo wazi sana, hata itikadi za mapinduzi zaidi zitafikia tu mabadiliko ya mabwana.” Hatimaye, na labda hiki ndicho kifungu kinachokumbukwa zaidi katika barua hiyo, Papa anaelezea kuunga mkono kwake chaguzi nyingi za kisiasa kwa Wakristo, bila kuathiri kujitolea kwake kwa kanuni za kiinjili: “Katika hali halisi na kwa kuzingatia mshikamano unaopatikana na kila mtu, aina mbalimbali halali za chaguzi zinazowezekana lazima zitambuliwe. Imani ile ile ya Kikristo inaweza kusababisha ahadi tofauti.”

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here.

 

14 Mei 2026, 09:58