Bendera za  dunia. Bendera za dunia. 

Umoja wa Mataifa unaadhimisha miaka 80 ya kuzaliwa:hebu tushikamane na tukidhi ahadi yetu ya kipekee ya UNwetu!

Leo ni siku rasimi ya kukumbuka siku ya kuzaliwa kwa Chombo cha Kimataifa cha Umoja wa Mataifa(UN)kunako tarehe 24 Oktoba 2025.Katika fursa hiyo Katibu Mkuu wa UN Bwana Guterres alituma ujumbe kwa njia ya video akihimiza“Mataifa yote kutoa kipaumbele cha kushirikiana pamoja katika kuendeleza majumu umoja huo kwa sababu ya kujisikia kuwa ni lao.”Hebu tuoneshe dunia kile kinachowezekana pindi ‘sisi watu’ tunapoamua kuchukua hatua pamoja."

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Katika fursa ya siku ya Umoja wa Mataifa ya kutimiza miaka 80 tangu kuanzishwa kwake tarehe 24 Oktoba 1945, mara tu baada ya vita vikuu vya II vya Ulimwengu, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) Bwana António Guterres, alituma ujumbe wake kwa njia ya  Video huko jijini New York Marekani,  katika Makao Makuu ya Umoja akisema kwamba “wakati wa kuundwa shirika hilo watu wote walizingatiwa na wote kupewa majukumu: “Sisi watu wa Umoja wa Mataifa... Haya si maneno tu ya utangulizi wa Chata ya Umoja wa Mataifa ni maneno yanayotuainisha sisi ni akina nani.”

Umoja wa Mataifa i zaidi ya Taasisi

Kiongozi huyo alisisitiza kuwa “Umoja wa Mataifa ni zaidi ya taasisi. Ni ahadi inayoishi ikivuka mipaka, ikiunganisha mabara, ikihamasisha vizazi. Kwa miaka themanini, tumefanya kazi kujenga amani, kukabili umaskini na njaa, kuhamaisha haki za binadamu, na kujenga dunia iliyo endelevu zaidi  kwa pamoja.” Akiakisi siku zijazo, Bwana Gutterres alisema: “tunavyoangalia mbele, tunakabiliwa na changamoto kubwa: mizozo inayoongezeka, hali ya  tabianchi, teknolojia za hali ya juu, na tishio la muundo wa taasisi yetu.

"Sisi Watu wa Umoja wa Mataifa", Gutterres

Bwana Gutterres alisema "Huu si wakati wa uoga au kurudi nyuma. Sasa, kuliko wakati wowote ule, dunia lazima ijizatiti kutatua matatizo ambayo si taifa moja linaweza kutatua peke yake.  Alihitimisha ujumbe wake kwa kutaka “ushirikiano zaidi duniani huku watu wote wakitambua Umoja wa Mataifa ni wao. Katika siku hii ya Umoja wa Mataifa, hebu tushikamane na tukidhi ahadi yetu ya kipekee ya Umoja wenu wa Mataifa. Hebu tuoneshe dunia kile kinachowezekana pindi sisi watu tunapoamua kuchukua hatua kwa pamoja”.

Mkataba wa UN

Mkataba wa Umoja wa Mataifa ni muhimu kwa kudumisha amani na usalama wa kimataifa, maendeleo ya uhusiano wa kirafiki kati ya mataifa, na kukuza ushirikiano wa kimataifa. Umoja huu una umuhimu muhimu wa kiishara na kisheria, hasa kwa nchi zilizo ndogo, ambazo zinaona katika Mkataba huo kama chanzo cha utulivu na usalama dhidi ya utawala wa wenye nguvu zaidi. Zaidi ya hayo, Mkataba huo umechukua jukumu la msingi katika kuondoa ukoloni na katika kuhakikisha haki na utu wa binadamu.

Mkataba huo ulitiwa saini huko Mtakatifu   Francisco mnamo tarehe  26 Juni  1945, na nchi 50 kati ya 51 wanachama (Poland, ambayo haikuwepo kwenye mkutano huo, ilisainiwa mnamo Oktoba 1945) mwishoni mwa Mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Umoja huo wa  Kimataifa. Na kwa njia hiyo ulianza kutumika mnamo tarehe 24 Oktoba1945, baada ya kuidhinishwa na wanachama watano wa kudumu wa Baraza la Usalama (China, Ufaransa, Umoja wa Kisovieti, Uingereza, na Marekani) na na nchi nyingi zilizotia saini.

Vatican na Palestina zina wawakilishi wa Kudumu katika Umoja wa Mataifa

Kwa sasa, kuna nchi wanachama 193 wa Umoja wa Mataifa. Mataifa mengine mawili, Kiti Kitakatifu au Vatican na Palestina, yana hadhi ya Wawakilishi wa Kudumu.  Nchi hizi 193 ni wanashama wa Shirika hilo na zimepiga kura kukubali Mkataba wa Umoja wa Mataifa, zikikubali majukumu yanayoambatana nao.Wawakilishi wa  Kudumu kama Vatican na Palestina hushiriki katika shughuli za Umoja wa Mataifa lakini hazina haki ya kupiga kura katika Umoja huo.

24 Oktoba 2025, 09:34