Katibu Mkuu wa UN Bwana  Antonio Guterres. Katibu Mkuu wa UN Bwana Antonio Guterres.  (ANSA)

Katibu Mkuu wa UN atoa wito kusitishwa kwa mapigano na kuimarishwa diplomasia

Bwana Guterres,Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa alionya kuwa mgogoro unaoendelea Mashariki ya Kati unaelekea kuwa hatari zaidi huku ukitishia kugeuka kuwa vita pana yenye athari kubwa duniani.Alizungumza hayo na wandishi wa habari Aprili 2,jijini New York Marekani.Alisisitiza kuimarishwa kwa Diplomasia na kwamba atamtuma mjumbe wake Mashariki ya Kati.

Habari za Umoja wa Mataifa(UN).

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana António Guterres  alizungumza na waandishi wa habari jijini New York, Marekani, Alhamis tarehe 2 Aprili 2026  akieleza juu ya  mgogoro katika nchi za Mashariki ya Kati kuwa  sasa umeingia mwezi wa pili, na kusisitiza kuwa kila siku inayopita inaongeza mateso ya kibinadamu, uharibifu, pamoja na mashambulizi yasiyochagua walengwa. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa alibainisha kuwa raia na miundombinu ya kiraia wanaendelea kulengwa, hali inayoongeza hatari si tu kwa eneo hilo bali pia kwa dunia nzima. “Tuko ukingoni ‘kuingia’ vita vikubwa zaidi ambavyo vitaigharimu Mashariki ya Kati na kuwa na athari kubwa duniani,” amesema.

Athari za kiuchumi na kijamii zaanza kuonekana duniani

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, alieleza kuwa mgogoro huo tayari una athari za kimataifa, hususan kutokana na kuzuiwa kwa uhuru wa usafiri wa majini katika njia muhimu kama Mlango-bahari wa Hormuz. Alionya kuwa hali hiyo inaathiri zaidi mataifa maskini na watu walio hatarini, huku ikichangia kupanda kwa bei za chakula na nishati katika maeneo mbalimbali duniani, ikiwemo Ufilipino, Sri Lanka na Msumbiji.

Wito wa kusitishwa kwa mapigano na kuimarishwa kwa diplomasiaBwana Guterres alisitiza kuwa kuendelea kwa vita kutasababisha kuongezeka kwa maafa, akitoa wito wa kusitishwa kwa haraka kwa mapigano na kupewa nafasi juhudi za kidiplomasia zinazoendelea. Aidha, alisisitiza umuhimu wa kuheshimu sheria za kimataifa, ikiwa ni pamoja na Mkataba wa Umoja wa Mataifa, pamoja na kulinda uhuru wa mataifa na mipaka yao.

Mjumbe wake kwenye eneo la mgogoro

Katibu Mkuu pia alitangaza kumtuma mjumbe wake binafsi, Jean Arnault, kwenda katika eneo la mgogoro ili kusaidia juhudi za kutafuta suluhu ya amani. “Ninamtuma Mjumbe wangu Maalum Jean Arnault. Lengo ni kuunga mkono jitihada za kikanda. Lazima tupate njia ya amani ya kutoka katika hali hii.” Amesema Guterres.

“Chaguo la amani bado lipo”

Alihitimisha, Katibu Mkuu Guterres akisisitiza kuwa migogoro haiishi yenyewe bali humalizika pale viongozi ambapo wanapochagua mazungumzo badala ya uharibifu. “Chaguo hilo bado lipo  na lazima lifanywe sasa,”

Kuhusu suala la Finland

Katika kilele cha mgogoro, kuna jaribio la kwanza la kufungua tena mazungumzo ya kidiplomasia. Rais wa Finland Alexander Stubb alifanya mkutano wa moja kwa moja na Rais wa Iran Masoud Pezeshkian, akichunguza njia zinazowezekana za kujitenga. "Tulijadili hali nchini Iran na Mashariki ya Kati. Kusitisha mapigano na suluhisho la kidiplomasia vinahitajika haraka," Stubb aliandika katika ujumbe uliochapishwa kwenye X. Kiongozi huyo wa Finland pia alisisitiza hitaji la "kusimamisha mashambulizi dhidi ya nchi jirani na uzambazaji huru katika Mlango-Bahari wa Hormuz," mojawapo ya mambo nyeti zaidi ya kimkakati kwa biashara ya nishati duniani. Licha ya tofauti kubwa kati ya pande hizo, Stubb alisisitiza umuhimu wa kudumisha njia wazi za mawasiliano: "Ni muhimu kuendelea na mazungumzo."

Masoko yako katika Misukosuko

Katika nyanja za kiuchumi na kifedha, matokeo ya mvutano yalikuwa ya haraka. Kauli za Trump, ambazo zilizungumzia vita "karibu na mwisho wake" bila kutoa muda sahihi na kutabiri mashambulizi mapya, ziliwakatisha tamaa wawekezaji. Matokeo hayo yalikuwa mshtuko mkubwa kwa masoko ya kimataifa. Bei ya mafuta ilipanda hadi viwango vya juu vya rekodi. Brent crude, kiwango cha kimataifa, kilipanda hadi $109 kwa pipa mwezi Juni, na kuashiria ongezeko la 8%. Athari hiyo pia inahisiwa na watumiaji: Nchini Marekani, bei ya wastani ya petroli ilipanda hadi $4.08 kwa galoni, ongezeko la 37% tangu kuanza kwa mzozo. Bei ya dizeli ilipanda kwa kasi zaidi, na kufikia $5.51, hadi 47%.

Kuanguka kwa Soko la Hisa

Masoko ya hisa yaliitikia vibaya. Huko New York, faharisi ya S&P 500 ilipoteza 1.2% katika biashara ya mapema, na kurudisha nyuma faida ya siku iliyopita. Nchini Asia, Nikkei 225 ya Japani ilifunga kwa 2.4%, huku hisa za Korea Kusini zikionyesha utendaji mbaya zaidi, zikishuka kwa 4.5%. Barani Ulaya, Stoxx 600 ilishuka kwa 1.5%, huku kushuka kukiwa kumeenea katika masoko makubwa, kuanzia London hadi Paris hadi Frankfurt.

03 Aprili 2026, 10:12