Tafuta

2025.09.09 Padre Joseph Farrell ni Mkuu Mpya wa Shirika la Waagostinian duniani. 2025.09.09 Padre Joseph Farrell ni Mkuu Mpya wa Shirika la Waagostinian duniani.  

Padre Joseph Farrell ni Mkuu Mpya wa Shirika la Waagostinian

Ni katika uchaguzi uliofanyika alasiri tarehe 9 Septemba 2025 katika mchakato wa Mkutano Mkuu wa 188 wa Shirika la Mtakatifu Agostino.Alizaliwa miaka 62 iliyopita huko Pennsylvania nchini Marekani,ambaye ataongoza kwa miaka 6 ijayo Shirika la Mtakatifu Agostino duniani ambalo,Papa Leo XIV anatoka.

Vatican News

Padre Joseph Farrell kuanzia tarehe 9 Septemba 2025 ni Mkuu wa 98 wa Shirika la Mtakatifu Agostino, katika zaidi ya miaka 750  ya historia ya Waagostinian duniani. Alasiri hiyo walimchagua Ndugu waagostinian 73 wanaoshiriki Mkutano Mkuu wenye haki ya kupiga kura, waliounganika pamoja katika Mkutano Mkuu wa 188, ambao unaendelea jijini Roma katika Taasisi ya Kipapa ya Baba wa Kanisa Augustinianum.

Padre Joseph Farrell

Padre Joseph Farrell

Padre Farrell, ambaye kwa sasa alikuwa ni makamu wa Shirika na Msaidizi Provinsi ya Amerika Kaskazini, alipokea muhuri wa idhini kutoka kwa Padre Alejandro Moral Antón, ambaye amemaliza muhula wake wa pili, na kukubali jukumu lake jipya kama mkuu wa Shirika  hilo. Alizaliwa tarehe 11 Julai  1963, huko Drexel Hill, Pennsylvania, Marekani, na amekuwa anashirikiana na Provinsi ya Mtakatifu Agostino huko  Mtakatifu Thomas wa Villanova. Alihitimu  Shule ya Utawala wa Biashara katika Chuo Kikuu cha Villanova mnamo 1985. Miaka sita baadaye, alipata Shahada ya Uzamili wa Taalimungu katika Chuo Kikii Kishirikishi cha Taalimungu huko Washington. Alifunga nadhiri za kwanza katika Shirika mnamo 1987 na za daima  mnamo 1990.

Padre Farrell akiwa na Papa Leo
Padre Farrell akiwa na Papa Leo

Alipewa daraja la upadre  mnamo tarehe 29 Juni  1991, katika Kanisa la Mama Yetu wa Shauri Jema, huko Bryn Mawr, Pennsylvania. Alihudumu katika parokia, shule, na vyuo vikuu, akijitofautisha kama Padre wa chuo kikuu na profesa msaidizi huko Villanova, Marekani. Mnamo 2013, aliteuliwa kuwa makamu wa Shirika hilo, akimsaidia Mkuu wa Shirika hili  katika ziara za kisheria kwa jumuiya, mikutano ya shirika  na majukumu mengine. Mnamo 2019, alichaguliwa tena kama Makamu wa Shirika katika Mkutano Mkuu wa kawaida. Katika jukumu hili, alishirikiana kikamilifu na tume kadhaa za kimataifa za Shirika hilo huku  akitembelea jumuiya za Kiagostinian katika nchi mbalimbali.

10 Septemba 2025, 09:28