Maaskofu wa Ulaya na Afrika wakutana Luxembourg:'Uinjilishaji na Sinodi:Njia za Bara'
Vatican News
Kuanzia tarehe 25 hadi 28 Mei 2026, ujumbe wa maaskofu kutoka Shirikisho la mabaraza ya Maaskofu wa Ulaya (CCEE) na kutoka Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu wa Afrika na Madagascar(SECAM) watakutana huko Luxembourg kwa ajili ya Semina kuhusu: "Uinjilishaji na Sinodi: Njia za Bara." Semina hiyo itafanyika ikifuatia na ilie ya mnamo mwaka 2004 ili kutoa fursa muhimu kwa ajili ya kubadilishana taarifa na kutafakari kwa pamoja kuhusu changamoto zinazolikabili Kanisa duniani, na italenga mwaka huu 2026 kuchunguza awamu ya utekelezaji wa Sinodi na maendeleo yanayofanywa katika Makanisa mahalia pamoja na changamoto za uinjilishaji katika miktadha tofauti ya bara kwa kuzingatia Wosia wa Baba Mtakatifu Francisko wa Evangelii Gaudium yaani Injili ya Furaha uliochapishwa tarehe 24 Novemba 2013.
Ratiba ya tarehe 25 Mei 2026
Ratiba itaanza Jumatatu tarehe 25 Mei 2026 kwa ziara ya Tamasha la kiutamaduni la Echternach katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Willibrord. Sherehe ya uzinduzi itaongozwa na Askofu Heiner WILMER, SCJ, wa Jimbo la Münster na Rais wa Baraza la Maaskofu wa Ujerumani.
Tarehe 26 Mei 2026
Siku ya Jumanne tarehe 26 Mei, washiriki watahudhuria Misa Takatifu katika Abasia ya Echternach, ikiongozwa na Kardinali Ladislav NEMET, SVD, Askofu Mkuu wa Belgrade na Makamu Rais wa CCEE, na kutakuwa na maandamano maarufu ya ngoma ya kiutamaduni ya Echternach (Iechternacher Sprangprëssioun), ambayo ni ibada ya Mtakatifu Willibrord na imesajiliwa kwenye Orodha ya Wawakilishi wa Urithi wa Utamaduni Usiogusika wa Binadamu. Alasiri hiyo hiyo, shughuli zitaanza na salamu za ufunguzi na utangulizi kutoka kwa Askofu Mkuu Gintaras GRUŠAS, wa Vilnius na Rais wa Shirikisho la Mabaraz aya Maaskofu Ulaya (CCEE,) na kwa Kardinali Fridolin AMBONGO, OFMCap., Askofu Mkuu wa Kinshasa na Rais wa Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu Afrika na Madagascar(SECAM.) Hii itafuatiwa na utambulisho wa washiriki kutoka kwa vyombo viwili vya Kanisa.
Tarehe 27 Mei 2026
Jumatano tarehe 27 Me, siku itaanza na Misa Takatifu ikiongozwa na Kardinali Fridolin AMBONGO, OFMCap. Vikao vya kazi vitajikita na "Awamu ya Utekelezaji wa Sinodi kuhusu Sinodi." Miongoni mwa hotuba zitakazotolewa ni pamoja na ile ya Kardinali Jean-Claude HOLLERICH, SJ, Askofu Mkuu wa Luxembourg na Makamu Rais wa Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu Ulaya (CCEE,) kuhusu Timu ya Sinodi ya wajumbe wa kitaifa wa Ulaya, na ile ya Askofu Lucio Andrice MAUNDULA, wa Jimbo la Chimoio na Mratibu wa Timu ya Sinodi ya Afrika. Hizi zitafuatiwa na mawasilisho kutoka kwa Kardinali Ladislav NEMET, SVD, kuhusu Kikosi Kazi cha Sinodi ya Ulaya, na kutoka kwa Askofu Mkuu Anthony MUHERIA, wa Jimbo Kuu la Nyeri na Makamu Rais wa Shirikish la manbaraza ya Maaskofu wa Afrika Mashariki AMECEA, ambaye hotuba yake itajikita kwa kazi ya sinodi katika muktadha wa Afrika na kwa desturi bora za kichungaji. Alasiriy a siku hiyo, kutakuwa na vipindi vya "Mazungumzo katika Roho" na majadiliano ya jumla.
Tarehe 28 Mei 2026
Siku ya mwisho, Alhamisi tarehe 28 Mei, itatengwa kwa ajili ya Waraka wa “Evangelii Gaudium” na mada ya uinjilishaji katika muktadha wa Ulaya na Afrika. Wazungumzaji watakuwa Askofu Alexandre JOLY, wa Jimbo la Troyes, na Askofu Mkuu José Manuel IMBAMBA, wa Jimbo Kuu la Saurimo na Makamu wa Pili wa Rais wa SECAM. Semina hiyo itahitimishwa kwa kazi ya kikundi, muhtasari wa mwisho na Maadhimisho ya Misa Takatifu ikiongozwa na Askofu Gintaras GRUŠAS, Rais wa CCEE.
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here.