Uwepo wa uinjilishaji wa watawa katika mitandao ya sasa ya kidijitali!
Na Sr. Alejandra Treviño, FMA.
‘Mpango wa Fiat’ ulianza mwaka 2017 wakati wa mkutano wa Baraza la Maaskofu Katoliki wa Marekani kwa viongozi Wakatoliki. Katika mkutano huo, Sr. Bernadette Mota, FMA, na Sr. Phuong Nguyen, FMA, Shirika la Mabinti wa Maria Msaada wa Wakristo(FMA) kutoka Mkoa wa Magharibi mwa Marekani, walijifunza kuhusu ‘Kundi la Samuel,’ Mpango mwingine wa utambuzi kwa vijana ulioanzia nchini Italia kupitia ‘Mitume wa Maisha ya Ndani.’ Mwishoni mwa mwaka huo, Masista walianzisha ‘Kundi la Samuel’ katika Jimbo la Colorado Springs. Sr. Linda Gonzalez, FMA, alijiunga na timu inayoongoza programu hiyo hivi karibuni. Kufikia Machi 2019, mpango huo ulikuwa unastawi, hata hivyo, janga la Uviko19 lilisimamisha ghafla mikusanyiko yote ya ana kwa ana.
Mbinu ya kidijitali ya ubunifu katika huduma
Ukweli mpya uliwatia moyo watawa hawa kukusanyika mtandaoni na kufikiria njia mbadala ya kuwaongoza vijana katika utambuzi wao wa kitaaluma. Sr. Sydney Moss, FMA, Mkurugenzi wa Miito wa Jimbo la Magharibi mwa Marekani wa Masista, hao anatafakari kuhusu ukweli kwamba "wakati wa janga hilo, tulipolazimika kubadilika na kutafuta mbinu tofauti ya huduma, ilikuwa kazi ya Roho Mtakatifu kuja na wazo la “Mpango wa Fiat.”
Kundi la Samuel lilibadilika na kuwa kile ambacho sasa ni Mpango wa Fiat, likijumuisha sehemu ya mwisho ya miezi mitatu ya Kisalesian inayojikita hasa na maisha ya kitawa kwa kutumia kitabu cha Sr. Clare Matthiass cha Mang’amuzi ya Maisha ya wito wa Utawa, jina la “Mpango wa Fiat” lilikuwa msukumo wa kuwatia moyo washiriki kusema "Tazama mimi hapa” yao wenyewe kama Mama Maria. "Kwa sababu ya mpango huu mpya, tumeweza kuwafikia vijana wa kike wengi zaidi kuliko kama tungeendelea kufanya mambo kwa njia ile ile."
Kuunda Jumuiya mpya
‘Mpango wa Fiat’ ni nafasi ya kuunda Jumuiya. Marylynn Alvarado, 2025-2026 Mshiriki wa Mpango wa Fiat alishirikisha jinsi "imekuwa nzuri sana kujua kwamba kuna wanawake wengine vijana ambao wako katika hali kama hizo, tuko pamoja ndani yake. Nimeingia katika Jumuiya hii kupitia mchakato wa utambuzi, si mimi mwenyewe. Nimeongozwa na Mungu, ninatembea na Kristo na siko peke yangu," alisisitiza
Mwelekeo mpya wa kiroho
Kama sehemu ya programu, washiriki wanaombwa kukutana na mkurugenzi wa kiroho mara moja kwa mwezi ili kushughulikia taarifa zinazoshirikishwa wakati wa kila kipindi. Lucia Martinez, mshiriki wa Mpang wa Fiat wa 2024-2025 alithibitisha kwamba "kivutio kikubwa kwangu kilikuwa kuongozwa kupitia mwelekeo wa kiroho, hasa na mtawa. Kusikia na kujifunza kutokana na uzoefu na hekima ya mtawa ilikuwa kitu ambacho kilinisaidia sana kuelewa jinsi Mungu alivyokuwa akitembea katika maisha yangu na kile ambacho ananita."
Kuondoa mawazo ya visumbufu
Naye Cecilia Garcia, akiwa tayari kutambua wito wake uliogawanywa kati ya ndoa na maisha ya Jumuiya, alishiriki katika mpango wa Fiat wa 2021-2022 kuhusu maisha, yaani, ana kwa ana, huko California, ambapo aliungana mtandaoni na washiriki wengine Marekani yote na nchi zingine. Kwa upande wake alisema, "Mpango wa Fiat uliniruhusu kupata nafasi ya kutulia kutoka katika ratiba yangu yenye shughuli nyingi kama mwanafunzi na kuondoa mawazo yangu ya usumbufu na kujaribu kusikia kile ambacho Mungu alitaka kutoka kwangu. Uliniruhusu kuunda njia iliyopangwa zaidi ya kutenga muda wa kuzungumzia miito tofauti na kutafakari Maandiko. Tulizungumza mengi kuhusu Mama Maria, na kile alichokuwa nacho, na karama za Roho Mtakatifu zinazokuja na kila wito."
Kugundua majeraha ya ndani
Wakati wa Mpango wa Fiat, watawa hujadili mambo yanayohusiana na utambuzi/ mang’amuzi, kujijua, uponyaji kutokana na majeraha ya ndani, na vipengele vingine tofauti vya maisha ya kitawa, kupitia mtandao (Zoom). Sehemu ya mtandaoni ya Mpango wa Fiat inaisha na kukutana kwa ana kwa washiriki. Nafasi hii ya nne, inayounganisha uzoefu wa kidijitali na uzoefu wa ana kwa ana, hutoa fursa ya kutoka katika ulimwengu na kukusanyika ana kwa ana baada ya miezi 8 ya kuwa pamoja katika nafasi ya kidijitali.
Ufahamu wenye nguvu
Kwa upande wa Courtney alitambua wito wake aliposhiriki katika Mpango wa Fiat ya 2024-2025 mtandaoni na ya ana kwa ana mwishoni. Alishirikisha jinsi ya kutafakari na mazungumzo ya watawa kulivyomsaidia katika harakati zake, akiakisi maarifa muhimu: "Moyo wako umeundwaje kupenda? Je, unahisi kama moyo wako umeundwa kumpenda mtu mmoja pekee? Ikiwa ndivyo, ndivyo Mungu anataka uwe Mtakatifu." Baada ya kuhudhuria mafungo ya ana kwa ana, aliamua kuchukua hatua inayofuata na kwa sasa yuko katika hatua ya kwanza ya malezi pamoja na Shirika la Mabinti wa Maria Msaada wa Wakristo(SMA).
Papa Leo XIV katika barua yake ya kitume ‘A Fidelity that Generates the Future’ yaani Uaminifu unaozaa Mustakabali, alibainisha kuwa: “Kila wito katika Kanisa hutokana na kukutana kibinafsi na Kristo, ambaye humpatia maisha yenye upeo mpya na mwelekeo thabiti.” Kabla ya kujitolea katika huduma yoyote, kuna sauti ya Mwalimu ikiita: “Njoo unifuate (Mk 1:17)." Kwa njia hiyo Masista wako katika mwaka wao wa 6 wa uinjilishaji uliojikita katika utamaduni wa kidijitali kupitia Mpango wa Fiat. Wanatoa nafasi ya maisha kwa vijana wa kike ili kuingia katika mchakato wa utambuzi wa miito yao. Kukutana kwa Masista na washiriki kupitia Mpango wa Fiat kunawezekana na wale wanaotoa sala zao kwa ajili ya miito mitakatifu ya ndoa na maisha ya kitawa, na wale wote ambao wameunga mkono mpango huo kifedha, hasa Taasisi Yetu ya Wageni wa Dominika (OSV) na Mfuko wa Scanlan.
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here.