Tafuta

Hija ya Kitume ya Papa Francisko Cyprus na Ugiriki:afla ya makaribisho na mkutano

Papa Francisko amefika huko AteneUgiriki Ijumaa tarehe 4 Desemba 2021 na kukaribishwa kwa afla fupi baadaye kufanya mkutano na viongozi wakuu na wa ngazi za kiraia pamoja na wanadiplomasia.Video fupi inaonesha tukio hilo la ziara ya Papa Ugiriki.

Na Sr. Angella Rwezaula – Vatican.

Papa Francisko akiwageukia viongozi wakuu wa Ugiriki katika hotuba yake ya kwanza mara baada ya kufika katika kisiwa hicho , siku ya Ijumaa tarehe 4 Desemba 2021, amewaalika wasiangukie kwenye ulaghai wa kimadaraka na sintofahamu za ubinafsi, badala yake wajikite kutibu na kuangaikia walio wadhaifu zaidi na utunzaji bora wa mazingira ambayo ni mambo makuu kwa ubinadamu uliopyaishwa katika bara. Na kuhusu wahamiaji, ni matarajio ya Baba Mtakatifu ya kuweza kuwa na  maono ya upamoja dhidi ya ubinafsi ambao unabagua. Video fupi inaonesha makaribisho akiwa tayari kwenye kisiwa hicho cha Ugiriki kuanzia tarehe 4 hadi 6 Desemba 2021.

Papa akihutubia huko Ugiriki
Papa akihutubia huko Ugiriki
Rais wa Ugiriki akihutubia
Rais wa Ugiriki akihutubia
Papa huko Ugiriki na mwenyeji wake
Papa huko Ugiriki na mwenyeji wake
04 December 2021, 14:55