Hija ya Kitume ya Papa Francisko Cyprus na Ugiriki:mkutano wa maaskofu,mapadre&watawa
Na Sr. Angella Rwezaula - Vatican.
Papa Francisko akiwa amefikia hatua ya pili ya ziara yake ya kitume, asubuhi tarehe 4 Dsemba ameondoka Cyprus kuelekea Ugiriki, ambapo kati ya mikutano aliyofanya katika siku hiyo ya kwanza Atene, amekutana pia na maaskofu, watawa, mapadre na makatekista katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Dionizi. Akizungumza nao, amewaomba wabariki kila kidogo katika utume wao kwani amesema kwamba hawakuombwa kuwa na roho ya kushindana au kusifika kidunia, badala yake wawe wakarimu katika kuinjilisha na sio kujaza vifaa huku wakibaki kushikilia majeraha ya wakati uliopita na kumbe badala yake wafanye kazi kwa ajili ya umoja kati ya Wakatoliki na Waorthodox. Video na picha zinaonesha wakati huu muhimu wa mkutano wao.