Tafuta

2025.09.11 Papa na maaskofu wapya kutoka Ulimwengu wa kimisionari. 2025.09.11 Papa na maaskofu wapya kutoka Ulimwengu wa kimisionari.  (@VATICAN MEDIA)

Papa Leo XIV,Maaskofu:Wawe na uhuru wa ndani,umaskini wa roho na utayari wa kutumikia

Papa Leo XIV alikutana mjini Vatican na Maaskofu waliowekwa wakfu mwaka uliopita,ili kushiriki katika kozi mbili za malezi na amekumbusha changamoto nyingi za kiutamaduni na kijamii zinazowakabili Maaskofu wapya:vita na ghasia,mateso ya maskini,matarajio ya dunia zaidi ya kidugu na msaada na thamani ya maisha.Baba Mtakatifu alikazia haja ya kutafsiri huduma ya mtu katika mtindo wa utume wa aina mbalimbali na wa kibunifu,kutegemeana na hali ilivyo.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Baba Mtakatifu Leo XIV  tarehe 11 Septemba 2025 alikutana katika  Ukumbi wa Sinodi, na maaskofu waliowekwa wakfu katika mwaka uliopita na wale wanaohudumu katika nchi za Kimisionari. Papa Leo  alizungumza kwa Kiingereza na Kiitaliano, na kutania kuhusu sauti yake kabla ya kuimba wimbo wa Uje Roho Mtakatifu  na pia aliakisi  hali ya mshangao ambayo bado ilionekana miezi minne baada ya kuchaguliwa kwake. "Nilifikiri, ningefika kwa kozi hii nikiwa nimevaa nguo nyeusi, pia." Kwa njia hiyo alihutubia maaskofu 192 kutoka mabara matano ambao tangu tarehe 3 Septemba, wamekuwa wakijishughulisha na mafunzo ya malezi yanayohamasishwa na Baraza la Kipapa la Uinjilishaji na Baraza la kipapa la Maaskofu. Maneno ya Papa yalihusu utambulisho wa askofu. Papa alionyesha mawazo yake mwenyewe na ya wale waliochaguliwa na kwamba labda baadhi yenu bado mnasema: 'Imekuwaje nilichaguliwa?' na Mimi, najiuliza."

Mkutano wa Papa na maaskofu wapya
Mkutano wa Papa na maaskofu wapya   (@VATICAN MEDIA)

Kwa njia hiyo Maaskofu waliowekwa wakfu wa uaskofu katika kipindi hiki cha  mwaka mmoja uliopita walihudhuria Kozi ya Malezi jijini  Roma, iliyohitimishwa siku ya Alhamisi tarehe 11 Septemba 2025 kwa kwa Mkutano katika Ukumbi wa Sinodi mjini Vatican alitoa hotuba yake, huku akiwaomba  Maaskofu wapya kukumbuka kwamba wamechaguliwa, wameitwa na kutumwa kuwa watumishi wa imani. "Ningependa kukumbuka jambo rahisi kama si la kuchukuliwa kuwa la kawaida: zawadi mliyopokea si kwa ajili yenu wenyewe, bali kutumikia kazi ya Injili.”

Baba Mtakatifu Leo XIV alijikita katika utume wa huduma waliokabidhiwa kwa Maaskofu, akisema unagusa utambulisho wao wenyewe. Utumishi, alisema, si tabia ya nje au seti ya matendo, bali ni mwito wa uhuru wa ndani, umaskini wa roho, na utayari wa utumishi unaotokana na upendo, ili kumwilisha chaguo la Yesu mwenyewe, ambaye alikuja kuwa maskini ili kututajirisha. Mungu alikuja kwetu si kwa nguvu bali kwa upendo wa Baba, aliongeza Papa, akibainisha kwamba “Mungu anatuita katika ushirika na Yeye mwenyewe.” Mtakatifu Agostino alisema kwamba Maaskofu, wanaosimamia wengine, ni lazima wajue kwamba wao ni “mtumishi wa wengi,” akielekeza kwenye onyo la Yesu kwa wanafunzi Wake ambao walikuwa wameanza kujitafutia ukuu.

Papa akihutubia maaskofu wapya
Papa akihutubia maaskofu wapya   (@VATICAN MEDIA)

Kwa hiyo “ninawaomba ninyi siku zote mkeshe na kutembea kwa unyenyekevu na sala, ili kujifanya watumishi wa watu ambao Bwana anawatuma ninyi kwao.” Papa Leo XIV alikumbuka maneno ya mtangulizi wake, Papa Francisko, aliyewaalika Maaskofu kukaribia kundi lao, kwani ukaribu wao unadhihirisha utunzaji wa Mungu kwa watu wake. Kama watumishi wa wote, Maaskofu wanapaswa kufahamu kwamba huduma yao inapaswa kumwilisha sura ya Kristo na huduma yake. Lakini, alibainisha Papa, lazima pia waunde utume wao ili kuakisi huduma ya Kristo, ikijumuisha katika njia yao ya uchungaji, kutangaza, na utawala.

Papa amekutana na maaskofu
Papa amekutana na maaskofu   (@VATICAN MEDIA)

Baba Mtakatifu Leo XIV katika hotuba yake alisisitiza kusema kuwa “Mgogoro wa imani na uenezaji wake, pamoja na ugumu wa kumiliki na utendaji wa kikanisa, unatualika kugundua tena shauku na ujasiri wa kutangaza Injili mpya.” Maaskofu aliongeza: “wanapaswa kuwakaribisha wale wanaobisha hodi kwenye milango ya Kanisa, bila kusahau changamoto nyingine ambazo ni za kitamaduni na kijamii zaidi, zikiwemo vita, ghasia, mateso ya maskini, changamoto za kimaadili, na tamaa ya dunia inayojikita katika misingi ya udugu na mshikamano.

Maaskofu wa kozi ya Malezi wamekutana na Papa
Maaskofu wa kozi ya Malezi wamekutana na Papa   (@VATICAN MEDIA)

Papa Leo alisema kuwa “Kanisa, linawatuma ninyi kama wachungaji wanaojali, wasikivu wanaojua jinsi ya kushiriki safari, maswali, mahangaiko, na matumaini ya watu; wachungaji wanaotamani kuwa viongozi, baba, na kaka kwa mapadre na kwa dada na kaka zetu katika imani.” Kwa kuhitimisha Baba Mtakatifu Leo XIV aliomba kwamba Maaskofu wapya wasikose kamwe upepo wa Roho, na kwamba furaha ya kuwekwa wao kwa, kama harufu nzuri, ipate pia kuenea juu ya wale unaoenda kuwatumikia.”

11 Septemba 2025, 15:41