Tafuta

2025.09.13  Papa akutana na washiriki wa Semina ya Kitaalimungu mjini Vatican. 2025.09.13 Papa akutana na washiriki wa Semina ya Kitaalimungu mjini Vatican.   (@Vatican Media)

Papa Leo XIV ahimiza wataalimungu kujibu changamoto za kidijitali

Papa alikutana takriban washiriki 130 wa semina ya"Uumbaji,Asili na Mazingira kwa Ulimwengu wa Amani,"iliyoandaliwa na Chuo cha Kipapa cha Taalimungu.Katika Hotuba aliwaalika kukuza taalimungu inayojikita katika kukutana kibinafsi na kuleta mabadiliko katika Kristo na yenye lengo la kujimwilisha katika matukio ya wanadamu wa leo hii:ukaribu,maumivu na furaha.Alihimiza kuendelea na njia ya mawazo iliyofuatiliwa na Mtakatifu Agostino,Thomas Aquinas na Mwenyeheri Rosmini.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Baba Mtakatifu Leo XIV alikutana mjini Vatican tarehe 13 Septemba 2025 katika  Ukumbi wa Clementine wa Jumba la  Kitume ya Vatican na Washiriki takribani 130 wa Semina ya kimataifa, iliyoandaliwa na Chuo Kikuu cha Kipapa cha Taalimungu, yenye mada “Uumbaji, Asili, Mazingira kwa Ulimwengu wa Amani.” Papa kwa njia hiyo aliwahimiza kufanya taalimungu ya hekima yenye uwezo wa kutoa majibu ya busara hata kwa changamoto za kidijitali. Katika hotuba yake, Baba Mtakatifu kwa mara ya kwanza alitoa muhtasari wa malengo ya Semina hiyo  iliyofanyika Alhamisi tarehe 11 na Ijumaa tarehe 12 Septemba 2025 katika ukumbi wa Casina Pio IV kwenye bustani nzuri za Vatican.

Washiriki wa Taalimungu wakutana na Papa
Washiriki wa Taalimungu wakutana na Papa   (@Vatican Media)

Semina hiyo ililenga  mada muhimu pia kwa watangulizi wake, Mtakatifu Yohane Paulo II, Benedikto XVI, na Francisko, kama vile uendelevu wa mazingira na ulinzi wa uumbaji. Baadaye alisisitiza jinsi  ambavyo juhudi ya kuboresha hali ya mazingira na kijamii ya ulimwengu wetu inahitaji kujitolea kwa kila mtu. Haja ambayo, kwa mujibu wa Papa, semina hiyo ilizingatia, na kupendekeza sahihi, kiutamaduni na kidini, mtazamo wa mshikamano na ushirikiano unaoshinda vikwazo na mipaka ya kikanda, kitaifa, kiutamaduni na hata kidini. Mtazamo huo, Papa Leo XIV aliendelea, unaakisi  mabadilishano makali zaidi na zaidi, na mipango ya kuvutia na yenye matunda. Taalimungu, ambayo ni kipimo cha msingi cha umisionari wa Kanisa na shughuli ya uinjilishaji Papa alitoa jukumu la kuendeleza tafakari hiyo. Kwa hakika kwa sababu inashughulikiwa kwa kila mtu katika kila zama, taalimungu msingi  ili kutimiza utume huu lazima uwe, katika maneno yaliyotungwa na Papa Francisko, yemye 'kutoka nje' yaani, yenye uwezo wa kuunganisha ukali wa kisayansi na shauku ya historia; taalimungu iliyojumuishwa, iliyojaa maumivu, furaha, matarajio, na matumaini ya wanadamu.

Papa autubia washiriki wa semina ya Taalimungu
Papa autubia washiriki wa semina ya Taalimungu   (@Vatican Media)

Papa Leo XIV alionesha mifano ya kihistoria ya Taalimungu ya hekima yenye uwezo wa kuunganisha mambo haya tofauti kwa mfano: "Mababa wakuu na Waalimu wa Mambo ya Kale," ambao walijua jinsi ya kuchanganya imani na sababu, kutafakari, sala, na Ibada kali.  Miongoni mwao, Mtakatifu Agostino, mfano wa wakati unaofaa, Papa alielezea kuwa, ni ambaye alikuza taalimungu  iliyoeleweka sio utafiti wa kufikirika, bali kama tunda la uzoefu wa Mungu na uhusiano muhimu na Yeye. Kwa njia hiyo  Askofu wa Hippo, alisema Papa leo XIV kuwa hasa katika Maungamo yake, alipendekeza tafakari ya kitaalimungu  iliyokuwa mwili na yenye uwezo wa kujibu mahitaji ya kiroho, mafundisho, kichungaji, na kijamii ya wakati wake. Kwa upande wa Mtakatifu Thomas kisha akaratibu safari ya Agostino ya kuwepo na yenye hisia kwa kutumia mbinu za Aristotle," akielewa taalimungu kama sayansi ya uelewa au hekima. Ukuzaji huu wa kiakili ulikamilishwa baadaye na Mwenyeheri Antonio Rosmini, ambaye, kama Papa  Leo XIV alivyosema, alichukulia Taalimungu kuwa usemi bora wa upendo wa kiakili.

Kisha Papa Leo alibainisha  juu ya changamoto za kidijitali kama mpaka unaofuata wa matumizi ya kazi ya kitaalimungu. Ushuhuda muhimu wa ujuzi wa imani katika huduma ya ubinadamu, katika nyanja zake zote: kibinafsi, kijamii, na kisiasa, ni Mafundisho ya Kijamii ya Kanisa, yanayoitwa leo hii kutoa majibu ya busara kwa changamoto za kidijitali pia. Katika utafutaji huu wa majibu, Taalimungu inapingwa moja kwa moja,kwa sababu mbinu ya kipekee ya kimaadili kwa Ulimwengu mgumu wa Akili Unde (AI) haitoshi."

Washiriki wa Semina ya Taalimungu
Washiriki wa Semina ya Taalimungu   (@Vatican Media)

Nidhamu ya hekima ina kazi ya kutoa maono ya kianthropolojia ambayo yana msingi wa hatua ya kimaadili. Ni muhimu, Papa alisema, kurejea swali la kudumu: mwanadamu ni nani, ni nini hadhi yake isiyo na mwisho, isiyoweza kupunguzwa kwa android yoyote ya kidigitali? Hatimaye katika  hotuba yake, Papa Leo XIV aliwahimiza Wataalimungu  kujihusisha sio tu na falsafa, bali pia na fizikia, biolojia, uchumi, sheria, fasihi, na muziki, ili kuleta chachu nzuri ya Injili kwa tamaduni mbalimbali na kukuza na kumwilisha taalimungu hii ya hekima, katika huduma ya Kanisa na ulimwengu wote.

Papa na Wataalimungu
13 Septemba 2025, 14:14