Tafuta

2025.10.03 Papa amekutana na Bi  Kerin Keller-Sutter, Rais wa Shirikisho la Uswiss. 2025.10.03 Papa amekutana na Bi Kerin Keller-Sutter, Rais wa Shirikisho la Uswiss.  (@VATICAN MEDIA)

Papa akutana na Rais wa Shirikisho la Uswiss

Papa Leo XIV alikutana mjini Vatican na Bi Karin Keller-Sutter mjini Vatican, asubuhi tarehe 3 Oktoba 2025.Baadaye ilifuatiwa na mkutano katika Sekretarieti ya Vatican ambapo kati ya masuala mengine ya Kimataifa,yale ya Ukraine na Gaza yamezungumzwa.

Vatican News

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ofisi ya Waandishi wa Habari ya Vatican ilibanisha kwamba Baba Mtakatifu Leo XIV,alikutana na  Rais wa Shirikisho la Uswiss, Bi Karin Keller-Sutter, asubuhi tarehe 3 Oktoba 2025, katika Jumba la Kitume mjini Vatican.

Papa na Rais wa Shirikisho la Uswiss
Papa na Rais wa Shirikisho la Uswiss   (@VATICAN MEDIA)

Bi Keller-Sutter baadaye alikutana na Kardinali Pietro Parolin, Katibu Mkuu wa Vatican, akifuatana na Askofu Mkuu  Paul Richard Gallagher, Katibu wa Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa. Majadiliano katika Sekretarieti ya Vatican yalilenga juu ya "mahusiano mazuri na yenye matunda ya nchi mbili," na "dhamira ya ukarimu na ya kitaaluma ya Walinzi wa Kipapa wa Uswisi" ilikumbukwa.

Picha ya Paomoja na wasindikizaji wa Rais wa shirikisho la Uswiss
Picha ya Paomoja na wasindikizaji wa Rais wa shirikisho la Uswiss   (@VATICAN MEDIA)

Matukio ya sasa pia yalijadiliwa, hasa masuala ya kimataifa na maeneo yenye maslahi ya pamoja, kwa kurejea hasa matarajio ya amani baada ya kumalizika kwa vita vya Ukraine na Gaza.

Rais wa Uswiss akisalimiana na Katibu Mkuu wa Vatican
Rais wa Uswiss akisalimiana na Katibu Mkuu wa Vatican   (@Vatican Media)

Kwa upande wa Zawadi Papa alimkabidhi Rais wa Shirikisho la Uswiss, Karin Keller-Sutter, bamba la shaba lililochongwa katika picha ya ushairi, mojawapo ya taswira zilizochorwa na Raphael Sanzio kwenye chumba cha kutia saini  katika Jumba la Kitume la Vatican kati ya 1508 na 1511. Sehemu ya mzunguko wa mapambo, Ushairi unashikilia kinubi na kitabu, alama za maelewano na uumbaji wa fasihi. Kimeandamana na makerubi wawili wenye maandishi "Numine Afflatur" ("Imeongozwa na Mungu"), usemi unaokumbuka imani ya kale kwamba ushairi si uwezo wa kibinadamu tu, bali ni zawadi iliyopuliziwa kutoka juu.

Wakati wa kubadilishana zawadi
Wakati wa kubadilishana zawadi   (@VATICAN MEDIA)

Wakati huo huo Rais wa Uswissi alimkabidhi Papa sanamu ya Mtakatifu Wiborada, mwanamke wa kwanza kutangazwa na Papa Clement II,  aliyemtangaza Mtakatifu katika sherehe kuu ya mnamo 1047 mbele ya Mfalme wa Ujerumani Henry III.

Bi Keller-Sutter na Papa
Bi Keller-Sutter na Papa   (@VATICAN MEDIA)

Wiborada alizaliwa katika familia yenye hadhi mwishoni mwa karne ya 9 huko Thurgau, Uswiss  ya leo, alijitolea maisha yake kuwatunza maskini na wagonjwa, na baadaye akaamua kustaafu maisha ya utawa katika moja ya Monasteri ya Mtakatifu Gallo. Aliuawa wakati alikuwa akisali mnamo Mei 926, wakati wa uvamizi wa Magyar. Anaoneshwa akiwa na  kitabu, kinachoashiria maandishi ya thamani ya maktaba ya monasteri  ambayo aliweza kuokoa kutokanana  na wavamizi, na halberd, na silaha ambayo ilitumika kumuua.

Asante sana kusoma makala hii, ikiwa unakata kubaki na masasisho zaidi, tunakualika kujiandikisha hapa: Just click here

 

03 Oktoba 2025, 14:00