Tafuta

2025.10.31 Wajumbe wa Shirika la Vyuo vikuu katoliki,Amerika Kusini na Visiwa vya Carribean. 2025.10.31 Wajumbe wa Shirika la Vyuo vikuu katoliki,Amerika Kusini na Visiwa vya Carribean.  (@Vatican Media)

Papa,Vyuo vikuu Katoliki:huduma kwa jamii,kuunda nafasi za kukutana kati ya imani na utamaduni

Katika hafla ya Jubilei ya Elimu,Papa leo XIV akikutana na Umoja wa Vyuo Vikuu Katoliki vya Amerika Kusini na Carribean alisisitiza kuunda raia wanaojitolea kwa wema wa pamoja na kuwahimiza wawe njia za akili kuelekea Mungu."Dhamira ya elimu ya juu ya Kikatoliki si kitu kingine ila kutafuta maendeleo fungamani ya mwanadamu,kuunda akili makini, mioyo inayoamini na raia waliojitolea kwa manufaa ya wote.Na haya yote kwa ubora,uwezo na weledi."

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Baba Mtakatifu  Leo XIV,  Asubuhi Ijumaa tarehe 31 Oktoba 2025  alikutana mjini Vatican Shirika la Vyo Vikuu Katoliki vya Amerika Kusini na Caribbean (ODUCAL). Hili ni Shirika linalokusanya zaidi ya Vyuo vikuu mia moja katika maeneo manne: Andes, BraziliKaskazini ya Cone, Mexico, Amerika ya Kati, na Carribbean. Mkutano huo unaambatana na Jubilei ya Ulimwengu wa Elimu, "ishara inayoonekana ya vifungo vya ushirikiano na mapenzi ambayo lazima yaeleze Shirika lenu,"alisema katika hotuba yake kwa lugha ya Kihispania. 

Katika hotuba yake alianza na salamu na kuwakaribisha, na kwamba angezungumza kidogo ili kuacha muda  kumsalimia kila mmoja na kuishi kidugu katika muktadha wa Jubilei, kwa uwepo wao hapa Roma. Namsalimu rais wa Shirika la Vyuo Vikuu vya Kikatoliki vya Amerika Kusini na Caribbean, Padre Anderson Antonio Pedroso, S.J., na wanachama wote wa ODUCAL, ambao, katika majukumu mbalimbali, wanatumikia misheni ya kielimu ya Kanisa. Hija ya kufika Roma, wakati wa Jubilei ya Ulimwengu wa Elimu, ni ishara inayoonekana ya vifungo vya ushirikiano na upendo ambavyo lazima viwe sifa ya shirika lenu."

Wajumbe kutoka Vyuo Vikuu vya Amerika Kusini
Wajumbe kutoka Vyuo Vikuu vya Amerika Kusini   (@Vatican Media)

Papa alisema kuwa "Mnajua kwamba, miongoni mwa malengo ya mtandao huu wa taasisi zaidi ya mia moja, ni kuendeleza elimu ya juu ya Kikatoliki na huduma ya jamii, kuunda nafasi za kukutana kati ya imani na utamaduni, kutangaza Injili katika mazingira ya chuo kikuu. Hija hii ya pamoja tayari inazungumza mengi, kwani inaelezea dhamira ambayo chuo kikuu kilizaliwa ndani ya Kanisa Katoliki: kuwa "kitovu kisicho na kifani cha ubunifu na usambazaji wa maarifa kwa ajili ya mema ya ubinadamu"(Mtakatifu Yohane Paulo II, Katiba ya Kitume Ex Corde Ecclesiae, nambari 1), ambapo "juhudi za pamoja za akili na imani zinawawezesha wanaume na wanawake kufikia kipimo kamili cha ubinadamu wao" (na.5)."

Wajumbe vya Vyo vikuu amerika Kusini
Wajumbe vya Vyo vikuu amerika Kusini   (@Vatican Media)

Leo, Chuo Kikuu Katoliki—kama Papa Francisko alivyosema—kinaendelea kuwa mojawapo ya vyombo bora zaidi ambavyo Kanisa hutoa kwa enzi yetu, na ni usemi wa upendo huo unaohamasisha kila tendo la Kanisa, yaani, upendo wa Mungu kwa mwanadamu (Papa Francisko Hotuba kwa Ujumbe wa Shirikisho la Kimataifa la Vyuo Vikuu vya Kikatoliki, Januari 19, 2024). Kutoka asili ya maisha ya chuo kikuu huko Amerika Kusini, Kanisa limekuwa nguvu inayoendesha elimu. Vyuo vikuu vya kwanza vya bara—kama vile Mtakatifu Domingo, Mtakatifu Marco wa Lima, Mexico, na vingine vingi, vilizaliwa kutokana na mpango wa maaskofu, watawa, na wamisionari walioamini kwamba kumtangaza Yesu Kristo, "Njia, Kweli, na Uzima" (Yh 14:6), "ni sehemu muhimu ya ujumbe wa Kikristo wa wokovu" (Papa Francisko, Hotuba kwa Washiriki katika Mkutano Mkuu wa Usharika wa Elimu ya Kikatoliki, Februari 20, 2020).

Wajumbe wa Vyuo Vikuu Amerika Kusini
Wajumbe wa Vyuo Vikuu Amerika Kusini   (@Vatican Media)

Vyuo vikuu mnavyowakilisha, vikiongozwa na imani hiyo hiyo, "vinaitwa kuwa 'safari ya akili kuelekea Mungu'" (Papa Leo XIV, Ujumbe kwa washiriki katika Mkutano Mkuu wa 28 wa Shirikisho la Vyuo Vikuu Katoliki vya Italia, Julai 21, 2025), hivyo kujumuisha utambulisho wa Kikatoliki ambao lazima uvitofautishe. Dhamira ya elimu ya juu ya Kikatoliki si nyingine ila kutafuta maendeleo fungamani ya mwanadamu, kuunda akili muhimu, mioyo inayoamini, na raia waliojitolea kwa manufaa ya wote. Na haya yote, kwa ubora, uwezo, na taaluma. Mnajua vyema changamoto zinazokabili elimu leo hii. Kwa ubunifu, na kujua kwamba neema inawategemeza, endeleeni  katika utume ambao Kanisa limewakabidhi." Papa aliwashukuru  kujitolea kwao na kazi yao yote katika kutekeleza kazi hii kubwa, na aliwakabidhi  kwa Bikira Maria, Kikao cha Enzi cha Hekima, ili, kama yeye, wawe watiifu kila wakati kwa tendo la Yeye ambaye ni Hekima yenyewe, Yesu Kristo Bwana wetu. Mungu awabariki.

Wajumbe wa vyuo vikuu vya Amerika kusini
31 Oktoba 2025, 10:45