Tafuta

2025.11.14 Papa azindia kituo kipya cha Afya cha Mtakatifu Martino mjini Vatican. 2025.11.14 Papa azindia kituo kipya cha Afya cha Mtakatifu Martino mjini Vatican.  (@Vatican Media)

Papa azindua Kituo cha Wagonjwa wa Nje cha Mt.Martino mjini Vatican

Papa Leo XIV alitembelea kituo kupya kilichofunguliwa hivi karibuni chini ya Nguzo za Basilika ya Mtakatifu Petro,ambacho kinapanua huduma za afya kwa maskini, ikiwa ni pamoja na kitengo cha X-ray ili kugundua haraka baadhi ya magonjwa ya kawaida yanayowaathiri watu wanaoishi mitaani.

Vatican News

Kituo kipya kimefunguliwa miaka kumi tu,  baada ya uzinduzi wa Zahanati ya Madre di Misercordia yaani "Mama wa Huruma" ambayo pia ipo karibu na Uwanja wa Mtakatifu Petro, kabla ya Siku ya Maskini Ulimwenguni itakayoadhimishwa Dominika, tarehe 16 Novemba 2025. Mara baada ya uzinduzi wa Mwaka wa Masomo katika Chuo Kikuu cha Kipapa cha Lateran, 2025/ 2026,  Ijumaa tarehe 14 Novemba, Baba Mtakatifu Leo XIV, alirudi mara moja mjini Vatican, yapata saa sita mchana, na kufikia eneo hilo la Mtakatifu Martino, lililo karibu na nguzo za Bernini, lilojulikana kwa kuwakaribisha maskini. Hapa, kuna mahali pa kuoga kwa wasio na makazi, eneo la kunyolea nywele, na Zahanati ya Mama wa Huruma, ambayo Papa Francisko aliiunga mkono kwa nguvu kutoa huduma kwa wale wasio na hati, fedha, au ufikiaji wa mfumo wa huduma ya afya, kitaifa.

Papa akibariki kituo kipya cha afya
Papa akibariki kituo kipya cha afya   (@Vatican Media)

Kituo cha kwanza cha ziara ya Papa Leo XIV  kilikuwa Zahanati  yenyewe. Akiongozana na Mhudumu Mkuu, yaani Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Huduma ya  Upendo, Kardinali Konrad Krajewski, alikutana na Dk. Massimo Ralli, Mkurugenzi wa Zahanati ya Wagonjwa wa Nje ya Baraza la Kipapa la Upendo, na Dk. Luigi Carbone, Mkurugenzi wa Afya na Usafi katika Gavana ya Jiji la Vatican. "Ilikuwa ziara ya faragha," Kardinali alisema, "kwa sababu hakuna mtu aliyeambiwa kwamba Papa anakuja, kwa hivyo ni madaktari waliokuwa tu katika  zamu waliokuwepo."

Papa akipata maelezo kuhusu kituo kipya cha afya
Papa akipata maelezo kuhusu kituo kipya cha afya   (@Vatican Media)

Siku ya Ijumaa asubuhi, Novemba 14, kulikuwa na madaktari wapatao 8, wauguzi 4, na watu 2 wa kujitolea, ambao tayari walikuwa wamewasaidia watu 65 kufikia wakati ambao Baba Mtakatifu aliwasili. Papa Leo XIV aliwasalimia na kuwauliza kuhusu shughuli za  Zahanati hiyo.

Sehemu za madawa
Sehemu za madawa   (@Vatican Media)

Huduma ya afya ya akili

Kardinali Krajewski alisisitiza jinsi ambavyo "Papa alivyoshangazwa na ukweli kwamba miongoni mwa madaktari waliokuwepo, pia kulikuwa na wataalamu wa magonjwa ya akili. Maskini wetu pia wanahitaji aina hii ya huduma, ambayo ni ngumu sana, kwa sababu mfupa unapovunjika, tunakimbilia mara moja kwenye chumba cha dharura," alisema, akiongeza kuwa "linapokuja suala la afya ya akili, kila kitu kinakuwa kigumu zaidi."

Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Huduma ya Upendo akitoa maelezo ya kituo hicho
Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Huduma ya Upendo akitoa maelezo ya kituo hicho   (@Vatican Media)

Madaktari wanatoka Hospitali ya Gemelli na hutoa utaalamu wao kwa kujitolea na uvumilivu. "Wana mengi ya kufanya hapa kwa sababu watu wanawaamini," Kardinali aliongeza. "Hatuombi hati, na labda hiyo inathibitisha heshima yao," alisema, akibainisha kuwa hawaonekani, kama wanavyokuwa mitaani mwa Roma kila wakati, "lakini hapa, msaada unazidi jina na nchi ya asili. Hapa, muhimu ni hitaji lako."

Papa akiwasalimia madaktari katika kituo kipya Mtakatifu Martino
Papa akiwasalimia madaktari katika kituo kipya Mtakatifu Martino   (@Vatican Media)

Huduma mpya

"Kazi nzuri, na asante," Papa Leo alisema, huku akitazama nje ya dirisha dogo karibu na bafu, akiwaacha wafanyakazi wakiguswa na ishara yake. Kisha aliwashukuru wale waliofanya kazi katika ukarabati wa Zahanati ya Wagonjwa wa Nje ya Mtakatifu  Martino, ambayo, kulingana na taarifa kutoka  Baraza la  Kipapa la Huduma ya Upendo nsasa ina vyumba viwili vilivyo na teknolojia ya kisasa ya matibabu na idara ya radiolojia, yaani ya Picha au  X-ray. Mashine ya X-ray ya kizazi kijacho itafanya iwezekane kugundua haraka na kwa usahihi visa vya nemonia, kuvunjika kwa mifupa, uvimbe, magonjwa ya kuzorota, mawe ya figo, na vizuizi vya utumbo, hali ambazo mara nyingi hupuuzwa miongoni mwa wale wanaoishi katika umaskini. Utambuzi huu wa mapema utawaruhusu madaktari kuanza matibabu yanayofaa haraka iwezekanavyo, na kusababisha ubora wa maisha kwa wale ambao hawana chochote.

Mashine za kisasa kwa ajili ya uchunguzi
Mashine za kisasa kwa ajili ya uchunguzi   (@VATICAN MEDIA)

Kumwona Yesu katika maskini

Zahanati mpya iliwezekana shukrani kutokana na ushirikiano na Kurugenzi ya Afya na Usafi ya Gavana wa  Jiji la Vatican na inatoa huduma kamili kwa wale wanaotafuta msaada wa kimatibabu.

Melezo kuhusu mashine za uchunguzi
Melezo kuhusu mashine za uchunguzi   (@VATICAN MEDIA)

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata taarifa mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku. Just click here

14 Novemba 2025, 16:08