Tafuta

2025.11.26 Papa wakati wa Katekesi. 2025.11.26 Papa wakati wa Katekesi.  (@Vatican Media)

Papa Leo XIV maombi ya sala zimsindikize katika ziara yake ya Turkiye na Lebanon

Papa atafanya ziara yake ya Kwanza ya Kitume,kuanzia,Novemba 27,ambayo mwishoni mwa katekesi,aliomba waamini wamwombee.Turkiye na Lebanon,"nchi atakazotembelea zina tajiri katika historia na kiroho."Papa pia alitangaza kuanza kwa Majilio Dominika ijayo Novemba 30 ambapo"Mama Kanisa anaanza mzunguko mpya wa kusherehekea mafumbo ya Kikristo.”

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Mara baada ya Katekesi yake, tarehe 26 Novemba 2025 Papa Leo XIV akiwa katika Uwanja wa Mtakatifu Petro kwa waamini na mahujaji waliofikia alieleza juu ya ziara yake ya kitume itakayo muona Nchi za Mashariki ya Kati kuanzaia tarehe 27 Novemba hadi Desemba 2. Kwa njia hiyo Papa alisema:  “Kesho nitasafiri kwenda Uturuki na kisha Lebanon kuwatembelea watu wapendwa wa nchi hizo, matajiri katika historia na mambo ya kiroho.” Kwa kuongeza “ Pia itakuwa fursa ya kuadhimisha miaka 1700 ya Mtaguso wa  kwanza la Kiekumeni ulioadhimishwa Nicea na kukutana na jumuiya ya Wakatoliki, kaka  na dada zetu Wakristo, na wale wa dini zingine. Ninawaomba mnisindikize kwa  sala zenu.”

Salamu binafsi mara baada ya katekesi
Salamu binafsi mara baada ya katekesi   (@VATICAN MEDIA)

Papa aliwasalimia mahujaji kwa lugha mbali mbali na kawa upande wa kiitalinao alisema: “Ninawakaribisha kwa dhati waamini wanaozungumza Kiitaliano, hasa wale kutoka parokia za Battipaglia, Sapri, na Vico Equense. Ninawasalimu waamini  wa Battenti ya Mtakatifu Filomena, Kwaya ya Mikono Mizungu ya Chiavari, Baraza la Kitaifa la Wataalamu wa Viwanda, Chama cha ANSI cha Faenza, na Chama cha ACAI cha Napoli.”

Picha binafsi na Papa
Picha binafsi na Papa   (@Vatican Media)
Salamu binafasi mara baada ya katekesi
Salamu binafasi mara baada ya katekesi   (@Vatican Media)

Papa aliongeza kusema kuwa “Ninawahimiza kila mtu kuendelea kwa kujitolea na ukarimu katika shughuli zao husika. Na hatimaye, nawasalimu wagonjwa, wenyendoa wapya, na vijana, hasa wanafunzi wa Mtakatifu Giovanni Rotondo na Triggiano.

Salamu binafsi mara baada ya katekesi
Salamu binafsi mara baada ya katekesi   (@VATICAN MEDIA)

Kipindi cha majilio

Dominika ijayo, tarehe 30 Novemba Kanisa litaanza tena mzunguko mpya wa kusherehekea mafumbo ya Kikristo,  katika Dominika ya kwanza ya Majilio. “Wakati huu wa mwaka unatuandaa kwa ajili ya Noeli ukiamsha kwa kila mtu hamu ya kukutana na Mungu anayekuja. Baraka zangu kwa wote!”

Kubariki mishumaa ya majilio binafsi na sanamu ya Maria
Kubariki mishumaa ya majilio binafsi na sanamu ya Maria   (@Vatican Media)
Salamu na zawadi binafsi baada ya katekesi
Salamu na zawadi binafsi baada ya katekesi   (@Vatican Media)
Baada ya Katekesi
26 Novemba 2025, 15:40