Tafuta

2025.11.27 Papa ameanza Ziara ya Kitume ya huko Türkiye  na Lebanon kwa kuondekea Uwanja wa Kimataifa wa Fiumicino,Roma-Ankara. 2025.11.27 Papa ameanza Ziara ya Kitume ya huko Türkiye na Lebanon kwa kuondekea Uwanja wa Kimataifa wa Fiumicino,Roma-Ankara.  (@VATICAN MEDIA)

Ziara ya Papa Leo XIV,kufika Ancara,Turkiye:Ni ziara ya I Kimataifa

Papa aliondoka uwanja wa ndege wa Fiumicino kuelekea Uturuki (Türkiye),kituo cha kwanza katika ziara yake ya kwanza ambayo itampeleka hata Lebanon kuanzia Dominika tarehe 30 Novemba hadi Jumanne tarehe 2 Desemba 2025.

Vatican News

Ziara yake ya kwanza ya kitume ya Papa Leo XIV imeanza, Alhamisi 27 Novemba 2025  ikimpeleka kwanza Uturuki (Türkiye), na ambapo atasimama Iznik, katika fursa ya maadhimisho ya miaka 1700 ya Mtaguso wa Kwanza wa Nicea. Ziara yake ya pili itakuwa Lebanon, kuanzia Dominika 30 Novemba 2025.

Il Pontefice all'interno dell'aereo, ad accompagnarlo anche l'immagine di Maria, Madre del Buon Consiglio

Papa ndani ya ndege, Picha ya Maria, Mama wa Shauri jema ikimsindikiza

Katika Ndege ya ITA Airways iliyomchukua Papa Leo, na msafara wake, na waandishi wa habari wengi, iliondoka saa 1:58 asubuhi masaa ya Ulaya kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Fiumicino. Imepangwa kuwasili Ankara, Turkiye(Uturuki,) saa 6:30 mchana, ambapo ataondoka jioni hiyo kuelekea Istanbul. Pia ndani ya ndege ya Papa kuna Picha ya Maria, Mama wa Shauri Jema iliyohifadhiwa katika Madhabahu ya Genazzano , madhabahi  inayohudumiwa  na Watawa wa Shirika la Mtakatifu Agostino.

Mnamo tarehe 10 Mei 2025, siku chache baada ya kuchaguliwa kwake, Papa Leo XIV  alifanya ziara ya ghafla kwenye Madhabahu hiyo mbali kidogo na  Roma. Baada ya kusali mbele ya picha ya Bikira, akiwasalimia wenzake, alisema kwamba ilikuwa ni hamu yake kuwa hapo wakati wa siku za kwanza za huduma mpya "ambayo Kanisa," aliongeza, "limenikabidhi, kuendeleza utume kama Mrithi wa Petro."

Leone XIV a bordo dell'aereo per il suo primo viaggio apostolico , prima tappa la Turchia

Leo XIV akiwa ndani ya ndege kwa ziara  yake ya kwanza ya kitume, kituo cha kwanza Uturuki

Papa aliondoka Vatican yapata saa 1:00 asubuhi majira ya Ulaya na kusafiri kwa kuelekea Uwanja wa Kimataifa wa Ndege huko Fiumicino Roma. Papa Leo XIV anakuwa Papa wa tano kutembelea Turkiye(Uturuki,) na kauli mbiu ya Ziara  yake nchini humo ni "Bwana Mmoja, Imani Moja, Ubatizo Mmoja."

Papa anatimiza hamu ya Hayati Papa Francisko ya kwenda Uturuki aliyokuwa akitarajia mnamo Mei 2025, kufuatia ziara yake ya 2014, kwa ajili ya kumbukumbu ya miaka 1700 ya Mtaguso wa  Nicea.

Kivutio kitakuwa Iznik, katika uchimbaji wa akiolojia wa Basilika ya kale ya Mtakatifu Neophytos, ambapo Papa, pamoja na Patriaki wa Constantinople Bartholomew I, watasali na mapatriaki wapatao ishirini na wawakilishi wa makanisa ya Kikristo mbele ya sanamu za Kristo na Baraza zima.

Telegram kwenda Italia

Wakati wa safari ya ndege, Papa alituma telegram kwa Rais wa Jamhuri ya Italia, Bwana Sergio Mattarella, ambapo alisisitiza kwamba safari yake ilikuwa "kukutana na watu hao, hasa kaka na dada katika imani, kwa kuhimiza njia za amani na udugu." Papa Leo  XIV anatoa salamu na matashi mema ya dhati kwa maendeleo ya kiroho, kiraia, na kijamii ya nchi hiyo ya Italia.

Papa akiingia kwenye Ndege
Papa akiingia kwenye Ndege   (@VATICAN MEDIA)

Kwa upande wake, mkuu wa nchi ya  Italia alitoa shukrani zake, akituma ujumbe ambapo alisisitiza kwamba mikutano ijayo ya Papa "inaamsha hisia za matumaini na imani kwa wale wote wanaoshiriki kujitolea kwa heshima ya utu wa binadamu na haki ya msingi ya uhuru wa kidini. Katika misingi hii ya umoja wa mataifa na mazungumzo kati ya imani, matarajio ya kuishi pamoja kwa amani miongoni mwa watu pia yanapata msingi imara."

Papa akioanda ngazi za ndege
Papa akioanda ngazi za ndege   (@Vatican Media)

Rais Mattarella alielezea imani yake kwamba uwepo wa Papa Leo "utawafariji wanawake na wanaume wenye mapenzi mema wanaokataa vurugu na ukandamizaji, wakifanya kazi kila siku kunyamazisha silaha na kuhakikisha kwamba mazungumzo na kutafuta manufaa ya wote vinashinda." "Ni wakati wa kutamani amani na utulivu, unaoshirikishwa na watu wote, kutafsiriwa," Rais wa Jamhuri aliandika, "kuwa mipango thabiti. Uwepo wake nchini Uturuki na Lebanon bila shaka utaimarisha tena sababu ya umoja na undugu wa kibinadamu."

Ziara ya Papa nchini Urutuki

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata taarifa mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku:Just click here

27 Novemba 2025, 09:30