Tafuta

2025.08.02  Papa wakati wa mkesha wa Sala kwa ajili ya jubilei ya vijana huko Tor Vergata. 2025.08.02 Papa wakati wa mkesha wa Sala kwa ajili ya jubilei ya vijana huko Tor Vergata.  (@Vatican Media)

Papa atakutana na vijana wa Roma 10 Januari 2026!

Papa Leo anatarajia kukutana na vijana barubaru wa Roma katika Ukumbi wa Paolo VI,mjini Vatican siku chache baada ya kufungwa kwa Jubilei ya Matumaini.

Na Angella Rwezaula- Vatican

Tukio hilo la Jumamosi, tarehe 10 Januari 2025, saa 11:00 jioni katika Ukumbi wa Paulo VI mjini Vatican litakuwa lisilokosekana. Siku chache tu kabla ya mwisho wa Jubilei ambayo itahitimishwa rasmi siku ya Epifania ya Bwana kwa kufungwa  Mlango Mtakatifu wa Basilika ya Mtakatifu Petr, vijana wa kike na kiume, barubaru wa Roma watakutana na Papa Leo XIV na kusikiliza maneno yake.

Makundi mengi yatahudhuria

Hili lilitangazwa katika taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Vikariate ya Roma, ambayo inabainisha kuwa vijana wengi watahudhuria: kuanzia wanafunzi wa katekisimu hadi wale wanaokusanyika katika vikundi vya parokia, kutoka wanachama wa harakati na vyama hadi wale waliojiandikisha katika vilabu vya michezo vya Kikatoliki, hadi wanafunzi wa vyuo vikuu, na wale wanaoishi mbali na nyumbani katika vyuo vikuu ndani ya Jimbo Kuu.

Reina:"utakuwa wakati wa furaha"  

 Ataye wasindikiza katika mkutano huu maalum na Papa atakuwa  Kardinali Baldo Reina, Makamu wa Papa Jimbo Kuu la Roma  ambaye alitangaza mkutano huo wakati wa kipindi cha maombi cha "Usiku katika Kanisa Kuu" kunako Novemba 21 iliyopita, na ambaye alirejesha mwaliko huo katika barua yake: "Itakuwa wakati wa thamani na furaha," Kardinali aliwaandikia mapadre, "ambao ninawaalika kuhimiza ushiriki wa vijana wa parokia zenu, nikiwahimiza wauone kama fursa muhimu ya kusikiliza maneno ya Askofu wetu."

 Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku, bofya hapa tu:Just click here

19 Desemba 2025, 18:38