Tafuta

2025.12.18 Ziara katika Maktaba ya Seneti ya Jamhuri ya Italia("Giovanni Spadolini") 2025.12.18 Ziara katika Maktaba ya Seneti ya Jamhuri ya Italia("Giovanni Spadolini")  (@Vatican Media)

Papa atembelea maonesho ya Maktaba ya Seneti kuhusu Biblia ya Borso d’Este

Papa Leo XIV alitembelea Jumba la Minerva alasiri Desemba 18 na kuona maonesho ya Jubilei yaliyowekwa kwa ajili ya mabaki ya kale.Akiambatana na Kardinali Parolin,Katibu Mkuu wa Vatican alikaribishwa na Spika wa Bunge la Italia La Russa.Papa alifunua picha ya Mtoto Yesu katika katika Pango la Kuzaliwa kwa Yesu.

Vatican News

Papa Leo XIV alikula chakula cha mchana tarehe 18 Desemba 2025 katika Ubalozi wa Kitume katika Jamhuri ya Italia, kabla ya kuendelea alasiri  hadi Jumba la  Minerva, kwenye jengo la Maktaba ya Seneti ya Jamhuri ya Italia.

Papa alipewa zawadi ya kengele ya Bunge
Papa alipewa zawadi ya kengele ya Bunge   (@Vatican Media)

Alikaribishwa na Spika wa Bunge, Seneta Ignazio La Russa, akifuatana na Katibu Mkuu wa Seneti, Dkt. Federico Silvio Toniato. Katika Ukumbi wa Schedario, baada ya salamu fupi na Makamu wa Bunge, Wakuu wa Makanisa, na Marais wa Vikundi vya Seneti, Papa alifunua pazia lililowekwa juu ya sanamu ya Mtoto Yesu katika Pango la kiutamaduni la Kuzaliwa kwa Yesu.

Papa alifunua Pango la Kuzaliwa kwa Bwana
Papa alifunua Pango la Kuzaliwa kwa Bwana   (@Vatican Media)
Papa akitia saini
Papa akitia saini   (@Vatican Media)

Akiongozana na Spika wa Bunge pamoja na Katibu Mkuu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin, Papa alielekea kwa muda mfupi hadi Ukumbi wa Bunge, ambapo Maonesho ya Biblia ya "Borso d'Este" yanafanyika, kabla ya kurudi Vatican.

Papa akitazama onesho la Biblia ya Kale
Papa akitazama onesho la Biblia ya Kale   (@Vatican Media)
Papa katika Bunge la Italia
Papa katika Bunge la Italia   (@Vatican Media)

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata taarifa mpya kwa kujisajili kwenye jarida letu la kila siku,bonyea hapa: Just click here.

18 Desemba 2025, 18:44