Tafuta

Papa Leo XIV alisali katika bandari ya Beirut:Ukimya na mkumbatio kwa manusura

Baba Mtakatifu Leo XIV,katika siku yake ya mwisho nchini Lebanon alitembelea eneo la mlipuko wa kutisha mnamo Agosti 2020 ambao uliua zaidi ya watu 240 na kujeruhi 7,000.Papa alisali mbele ya mnara wa marumaru wenye majina ya wafu,mmoja baada ya mwingine.Aliweka shada la maua na kuwasalimu manusura na familia za waathiriwa.Kila mmoja alishikilia picha za jamaa zao waliopotea.

Vatican News

Katika siku yake ya Mwisho ya Ziara yake ya Kitume nchini Lebanon, Baba Mtakatifu Leo XIV, Jumatano tarehe 2 Novemba 2025 ilimwona akitembelea mahali ambapo pamekuwa mandhari ya waliokufa katika umbo la maghala makubwa yaliyopuka yakionekana kutokea angani, marundo vifusi, magari yaliyochomwa yakiwa yamerundikana juu ya kila mmoja. Ni katika bandari ya Beirut ambayo Papa Leo aliwasalimia watu  manusura na familia za waliokufa katika ajali hiyo mbaya iliyotokea ya mlipuko wa kutisha mnamo Agosti 2020 ambayo iliwaua zaidi ya watu 240 na kujeruhi 7,000.

Mnara wa kumbukumbu ya waliokufa kwa mlipuko
Mnara wa kumbukumbu ya waliokufa kwa mlipuko   (@Vatican Media)
Papa anasali katika mnara wa kumbu kumbu
Papa anasali katika mnara wa kumbu kumbu   (@Vatican Media)

Kwa hiyo Papa Leo aliwasalimia hawa mmoja baada ya mwingine, huku wakilia au mikono yao ikiwa  imefunika midomo yao, wote wakiwa wamejipanga mstari na sura zikionesha huzuni au machozi.

Ziara ya Kitume ya Papa Leo nchini Lebanon
Ziara ya Kitume ya Papa Leo nchini Lebanon   (@Vatican Media)

Kwanza, kabisa mara baada ya kufika Papa Leo, alisimama kusali mbele ya Mnara huo wa ukumbusho wa marumaru unaoorodhesha majina yote ya wale ambao maisha yao yaliuawa na mlipuko huo, ili kutoa heshima yao. Papa Leo XIV alisimama kwa muda mrefu akisali kwa kimya, huku mikono yake ikiwa imeshikamana mbele ya nguzo. Katika hatua fulani, alitazama juu na kuanza kutembea kuelekea kwenye mnara.

Papa aliweka shada la maua
Papa aliweka shada la maua   (@Vatican Media)

Alipiga magoti kuweka shada la waridi nyekundu, kisha alisimama tena na kufungua mikono yake, akiinua juu. Sala, baraka, yote kimya kimya. Mdomo wa Papa uliweza kuonekana ukisonga na ananong'ona kitu cha ukimya.

Wafiwa wakiwa na picha za ndugu zao
Wafiwa wakiwa na picha za ndugu zao   (@Vatican Media)
Wakati muhimu wa sala ya kimya kwa waathirika wa mlipuko huko Beirut
Wakati muhimu wa sala ya kimya kwa waathirika wa mlipuko huko Beirut   (ANSA)
02 Desemba 2025, 11:39