Papa Leo XIV:Tunaishi historia si ya zamani tu,bali tunaandika historia ya upendo!
Na Angella Rwezaula – Vatican.
Ukarimu wa kukaribishwa huyeyusha itifaki baridi ya kutojali kwa juu juu inayopenya mifupa na moyo. Kwa hivyo, wakati wa ziara ya Kichungaji katika parokia ya Moyo Mtakatifu wa Yesu huko Castro Pretorio mnamo tarehe 19 Januari 2014, Papa Francisko alielezea ukaribu wa busara na ujasiri unaoweza kupita hata hofu halali, ya jumuiya katikati ya Roma ambayo kila siku huwafikia wale wanaoishi kwenye "pembezoni"mwa kituo kikubwa, cha Rome Termini, ambacho huwaahidi kuondoka lakini huzuia matamanio yao. Tarehe 22 Februari 2026 Papa Leo XIV aliwasili katika Parokia hiyo hiyo tena kwa ziara ya pili kati ya tano za kichungaji ambazo Papa mwenyewe atazitimiza kwa Jumuiya za Parokia za Jimbo lake kuelekea Pasaka ya Bwana.
Baba Mtakatifu Leo XIV aliwasili baada kidogo ya saa 2.15 asubuhi na kuwasalimia waamini nje ya Kanisa kabla ya kuanza misa takatifu saa 3.00 asubuhi. Papa alianza kusema kuwa “ Habari za asubuhi na Dominika njema nyote! Habari za asubuhi! Ni kwa jinsi gani ilivyo nzuri! Na asanteni kwa ukaribisho wenu na furaha hii, ambayo, ikiwa ni siku ya Bwana, Dominika, inakumbusha siku ya Ufufuko, furaha ya tumaini letu. Na ingawa Dominika ya kwanza ya Kwaresima ni wakati wa maandalizi, wa uongofu, huu pia ni wakati wa furaha, kwa sababu sote tunajua kwamba Bwana anataka kutupokea, anataka kutukaribisha, kama Parokia hii! Ni vizuri sana kuwa mahali ambapo kila mtu anakaribishwa! Asante, asanteni kwa parokia hii! Jina lenyewe: "Moyo wa Yesu," "Moyo Mtakatifu,” linatukumbusha maana ya ishara ya moyo kwetu: ishara ya upendo, hisani, ya ukarimu huu usio na kikomo wa upendo wa Bwana.
Na asubuhi hii tunawaona watu kutoka nchi nyingi duniani kote, wote wamekusanyika hapa, wakiwakilisha umoja huu, ushirika, na udugu, kuishi pamoja, ambako Yesu pekee ndiye anayeweza kuwawezesha. Ni upendo wa Yesu, ni huruma yake ndiyo iliyotuita pamoja asubuhi ya leo. Na kwa hivyo mimi pia ninasema: "Asante, Bwana, asante, na karibu kwenye sherehe hii!"
Papa alisema tena "Pia ninawasalimu jumuiya ya Wasalesian na Masista Wasalesian waliopo hapa. Hebu tufikirie kuhusu historia ya Parokia hii, tukianza na Don Bosco, pamoja na Wasalesiani, na mtangulizi wangu, ambaye pia aliitwa Leo, Leo XIII. Tunaishi historia ambayo si ya zamani tu. Leo tunaandika historia kwa sababu bado tunataka kuishi kwa kutimiza utamaduni huu mzuri wa huduma, upendo, na kufanya kazi na vijana. Ni vizuri sana kuwaona watoto hawa wote hapa! Tuwapigie makofi kwao! Hebu tupate uzoefu wa furaha ya maisha: jinsi gani ilivyo nzuri kuwa hai, kuwa na zawadi hii ya maisha ambayo Bwana anatupatia. Matashi mema! Dominika njema."Papa alisisitiza.
![]()
Kituo cha Termini kuna sanamu kubwa ya Mtakatifu Yohane Paulo II
Hewa baridi inaumiza asubuhi. Kwenye Njia ya Marsala, ukumbi mkubwa unaoelekea kituo umezuiwa, lakini mtiririko wa waamini ulimiminika kwa wingi, ukijaza ua mbele ya Kanisa kuu. Bango la Njano na nyeupe, rangi za bendera ya Jiji la Vatican, limetundikwa hapa, likisomeka: "Karibu Papa Leo XIV." Likiwa limezungukwa na jopo linalomuonesha Papa mwenyewe mbele na Mtakatifu Yohane Bosco nyuma.
![]()
Bango kwa ajili ya Papa: Mtazamo wa kwanza wa waamini unaonesha kuunganishwa kwa "vipingamizi" vilivyopo
![]()
Wapo watawa kutoka makundi matatu ya Mashirika wanaohudhuria jumuiya ya parokia mara kwa mara: Binti za Maria Msaada wa Wakristo, Wamisionari Masikini wa Mtakatifu Clara wa Sakramenti Takatifu, na Wamisionari wa Kristo Aliyefufuka.
![]()
Watawa Wasalesiani kutoka Ufilippini
![]()
Watoto wakiwa anamsubiri Papa Leo XIV
![]()
Papa akiwabariki wanandoa wajao (@Vatican Media)
Kibao kimeandikwa: tutaoana je unaweza kutubariki?"
![]()
Papa miongoni mwa watoto wa Parokia (@Vatican Media)
Kulikuwa na watoto wa darasa la Pili wa Katekesimu.
![]()
Papa aliingia katika Kanisa Kuu (@Vatican Media)
Hasa katika msimu huu wa Kwaresima, tunaitwa kugundua upya neema ya Ubatizo, kama chanzo cha uzima kinachokaa ndani yetu na kinachotusindikiza kwa heshima kubwa kwa uhuru wetu.
![]()
Papa na, nyuma, Kituo cha Treni cha Termini cha Roma (@Vatican Media)
Kiukweli, kuna wanafunzi wengi vijana wa vyuo vikuu, wasafiri wanaokuja na kwenda kwa kazi, wahamiaji wanaotafuta ajira, na wakimbizi vijana ambao wamejikuta katika jengo lililo karibu, kutokana na mpango wa Wasalesiani, fursa ya kukutana na wenzao wa Italia na kutekeleza mipango ya ujumuishaji.
![]()
Papa akiwasalimia wanaparokia (@Vatican Media)
Baada ya misia Papa Leo alikwenda kwenye Kikanisa kidogo na kukutana na Jumuiya ya Wasalesiani na Baraza la Kichungaji kabla ya kurudi Vatican
![]()
Chaja kwenye basilika: Chaja haipo tena. Mtu aliifungua na kuiweka mfukoni mwake. "Nipigie simu baada ya miaka ishirini," aliimba Lucio Dalla. Mtu, huyo leo, tayari amepiga namba ya simu hiyo.
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku. Just click here
