Papa amteua Askofu Kamomoe kuwa Askofu wa Jimbo la Wote,Kenya
Vatican News
Baba Mtakatifu Leo XIV tarehe 13 Mei 2026, amemteua Askofu wa Jimbo la Wote nchini Kenya, Mwashamu Askofu Simon Peter Kamomoe, ambaye hadi uteuzi huo alikuwa Askofu Msaidizi na Msimamizi wa Kitume wa Jimbo hilo ambalo lilikuwa wazi.
Wasifu wake
Askofu Simon Peter Kamomoe alizaliwa tarehe 26 Novemba 1962 huko Gatundu ,Wilaya ya Kiambu, Jimbo Kuu la Nairobi, Kenya na kupewa daraja la upadre kunako tarehe 18 Juni 1994. Baba Francisko, alikuwa amemteua kuwa Askofu wa Kiti cha Tubune ya Numidia na Msaidizi wa Jimbo Kuu la Nairobi, tarehe 13 Februari 2024, na kuwekwa wakfu wa kiaskofu tarehe 6 Aprili 2024. Na kisha tarehe 5 Julai 2025, Baba Mtakatifu Leo XIV akamteua kuwa Msimamizi wa Kitume wa Jimbo la Wote, nchini Kenya.
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here.
