Tafuta

2026.06.07 Papa alikutana na wanashirika wa Kiagostinian katika Ubalozi wa Vatican jijini Madrid nchini Hispania. 2026.06.07 Papa alikutana na wanashirika wa Kiagostinian katika Ubalozi wa Vatican jijini Madrid nchini Hispania.  (@Vatican Media)

Papa Leo XIV,Agostinian:Ushirika na umoja uwe ishara katika ulimwengu wa kihistoria!

Dominika alasiri Juni 7 katika Ubalozi wa Vatican huko Madrid,Papa Leo XIV aliwapokea Mapadre 220 Waagostiniani kutoka jumuiya mbalimbali na wanashirika kadhaa wa familia ya Waagostinian nchini humo.Alishangazwa na vijana,taa ya asubuhi."Alitutia moyo na ujasiri wa kusonga mbele na kufanya kazi kwa bidii zaidi kwa ajili ya watu,"mmoja wa Mapadre alitoa maoni kuhusu mkutano huo.

Vatican News

Dominika alasiri tarehe 7 Juni 2026 kabla ya kufika kwenye Jengo la Uwanja wa Movistar jijini Madrid  kwa ajili ya Mkutano wenye mada: “kusuka mitandao na Ulimwengu wa Utamaduni, Sanaa, Uchumi, na Michezo," ikiwa ni siku yake ya Pili akiwa katika ziara yake ya 4 ya Kitume Baba Mtakatifu Leo XIV alikutana na takriban Mapadre wa Kiagostiniani 220 kutoka Jumuiya mbalimbali na wajumbe kadhaa wa familia ya Kiagostinian walioko Hispania.

Papa na shirika lake la Kiagostiniani
Papa na shirika lake la Kiagostiniani   (@Vatican Media)

Ofisi ya Habari ya Vatican ilitangaza hili kupitia chaneli yake ya Telegram, ikiripoti kwamba: “Baada ya salamu kutoka kwa Mkuu wa Kanda, Papa alitoa shukrani kwa wale waliokuwepo kwa fursa ya kukutana, huku akisisitiza jinsi ushirika na moyo wa umoja miongoni mwa waagostinian unavyoweza kuwa ujumbe kwa ulimwengu katika wakati huu wa kihistoria.”

Papa akizungumza na Waagostinian walioko Madrid
Papa akizungumza na Waagostinian walioko Madrid   (@Vatican Media)

Huu ulikuwa ni ujumbe wa kuwafikishia vijana, kama wale 600,000 waliokusanyika katika Uwanja wa Lima Jumamosi usiku tarehe 6 Juni 2026, ambao walishirikisha maswali yao na juhudi zao za kiroho. Na, akitaja uwepo wa dada zao watawa wa ndani, Papa Leo XIV alisisitiza "thamani ya wito wao, pia katika kutoa maana kwa vitendo vya kijamii, wakati ambapo ukimya na uwezo wa kuingia moyoni mwa mtu unapotea," Ofisi ya habari ilitaarifu.

Papa na waagostinian huko Madrid
Papa na waagostinian huko Madrid   (@Vatican Media)

Hatimaye kabla ya kuwasalimia mmoja mmoja, Papa Leo XIV aliwaalika waliokuwapo kusali pamoja sala ya Baba Yetu, na kuwapatia Baraka ya kitume.

Papa alikutana na wanashirika wenzake waagostinian huko Madrid
Papa alikutana na wanashirika wenzake waagostinian huko Madrid   (@Vatican Media)

"Vijana, ni  kama taa ya asubuhi"

"Wakati wa mkutano huu mzuri na kama wa kifamilia kweli, alizungumzia kwa undani mada ya utunzaji wa kichungaji, hasa huduma ya vijana," Padre José alitoa maoni yake kwa waandishi wa habari wa Vatican. "Papa Leo alivutiwa sana na vijana wa kiume na wa kike wa Hispania", kwa maana ya wale aliokutana nao usiku wa mkesha.

Papa na wanashirika wake
Papa na wanashirika wake   (@Vatican Media)

"Alituambia kwamba vijana ni kama taa ya asubuhi, 'nyota.' Kwa Kihispania, brillio - mng'ao. Mnaitaje kwa Kiitaliano?" Padre Herranz aliuliza. "Pia alizungumzia huduma ya vijana na kazi yote ambayo sisi Waagostinian tunafanya na vijana. Alitushukuru kwa kile tunachofanya hapa Hispania na kututia moyo na ujasiri wa kusonga mbele na kufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya watu wa Mungu," alisema Padre huyo.

Papa akizungumza na wanashirika wake
Papa akizungumza na wanashirika wake   (@Vatican Media)
Papa na wanashirika walisali sala ya Baba Yetu na kuhitimisha kwa Baraka
Papa na wanashirika walisali sala ya Baba Yetu na kuhitimisha kwa Baraka   (@Vatican Media)

Imesasishwa tarehe 7 Juni 2026, saa 2.00 usiku na Angella Rwezaula .

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here.

07 Juni 2026, 19:40