Tafuta

2026.06.06Askofu Osório Citora Afonso, wa Jimbo la  Quelimane msumbiji ameuawa. 2026.06.06Askofu Osório Citora Afonso, wa Jimbo la Quelimane msumbiji ameuawa. 

Uchungu wa Papa kufuatia kuuawa kwa Askofu wa Quelimane,Msumbiji

Katika ujumbe uliotolewa kupitia chaneli ya Telegram ya Ofisi ya Habari ya Kiti Kitakatifu Papa Leo XIV anawasilisha kwa ulimwengu mshtuko wake kuhusu mauaji ya Askofu Osório Citora Afonso wa Jimbo la Quelimane na Msimamizi wa Kitume wa Beira.Papa anajiunga na sala na watu wa majimbo na taifa zima la Afrika katika saa hii ya maombolezo.

Vatican News

"Papa Leo XIV alipokea  kwa huzuni kuhusu kitendo kikubwa cha vurugu kilichosababisha kifo cha Mwashamu Askofu Osório Citora Afonso wa Jimbo katoliki la Quelimane na Msimamizi wa Kitume wa Beira, na anajiunga katika sala na watu wa majimbo hayo na Msumbiji nzima katika saa hii ya maombolezo, ili Bwana awape faraja, ili awalinde kila mwanaume na mwanamke katika upendo wake na kuwazuia wenye vurugu."

Haya yalielezwa kupitia chaneli ya Telegram ya Ofisi ya Habari ya Kiti Kitakatifu, na Msemaji Mkuu Dk. Matteo Bruni akitoa habari kwa dunia nzima kuhusu huzuni wa Papa, akiwa katika ziara yake ya kitume nchini Hispania, kufuatia mauaji ya Askofu  aliyepatikana amekufa tarehe 6 Juni 2026 katika majengo ya makazi ya maaskofu huko Quelimane.

Risasi kifuani na moyoni

Kulingana na Baraza la Maaskofu na waandishi wa habari na maafisa wa Huduma ya Kitaifa ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Askofu huyo alipigwa risasi kadhaa zilizopigwa hadi kiwango cha kifuani na moyoni, bila kuacha njia ya kukimbia. Sababu za uhalifu huo mbaya bado hazijajulikana, na wachunguzi wanaanza kuchunguza.

Huzuni wa Maaskofu

Huzuni ya kifo hicho cha kusikitisha pia kilioneshwa, kwa niaba ya Kanisa lote la eneo hilo, na Askofu Mkuu  Inácio Saúre, wa Jimbo Kuu la  Nampula na Rais wa Baraza la Maaskofu wa Msumbiji, ambaye katika taarifa rasmi alitoa wito, katika wakati huu mgumu, "kwa imani na mshikamano wa kidugu."

Askofu  Citora Afonso, ambaye hadi kifo chake alikuwa  Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu, pia alihudumu kama afisa wa Baraza la Kipapa la Uinjilishaji, Kitengo cha Uinjilishaji wa Kwanza na Makanisa Mapya Maalum, kuanzia 2017 hadi 2023.

Rambirambi za Rais Chapo

Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Daniel Francisco Chapo, alionesha masikitiko na kutoa  rambirambi zake nyingi, ambaye alisisitiza kwamba "kifo cha askofu kinawakilisha hasara isiyoweza kurekebishwa si tu kwa jamii nzima ya Kikristo bali pia kwa jamii yote ya Msumbiji."

KIFO CHA ASKOFU MSUMBIJI

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here.

07 Juni 2026, 09:50