Tafuta

2025.05.13 Delegazione Bielorussa Giubileo Chiese Orientali

Jubilei ya Makanisa ya Mshariki katika Kanisa Kuu la Mt.Petro na Liturujia ya Ethiopia

Kard.Souraphiel,Askofu Mkuu wa Addis Abeba,aliongozia liturujia akiwa pamoja na Askofu Mkuu wa Asmara,Menghesteab Tesfamariam.Zilitolewa salamu kutoka kwa Kardinali Claudio Gugerotti,Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Makanisa ya Mashariki.

Vatican News

Sherehe muhimu sana katika fursa ya  Jubilei ya Makanisa ya Mashariki ambapo Jumatatu tarehe 12 Mei 2025: Ibada ya Kimungu ya utamaduni ya  Ibada ya Ethiopia ilishuhudiwa katika Kanisa la Kwaya ya Basilika ya Mtakatifu Petro ikiwa na Kanisa la Ethiopia na Kanisa la Eritrea. Ibada hiyo iliongozwa na Askofu Mkuu wa Addis Ababa, Kardinali Berhaneyesus Demerew Souraphiel, kwa kusaidiana na Askofu Mkuu wa Asmara, Menghesteab Tesfamariam.

Mwanzoni, mwa ibada hiyo, Kardinali Claudio Gugerotti, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Makanisa ya Mashariki alitoa salamu zake hapo na kuwashukuru wale waliofika katika hija ya maadhimisho ya Jubilei ya Matumaini 2025. Kardinali alifikisha ukaribisho na ukaribu wa Papa Leo XIV,  na kusema kuwa "ambaye hakika atatuongoza katika njia ya wokovu," huku akikumbuka kusindikizwa kwa miaka hii na Papa Francisko, pia hata kukumbatiwa na Kanisa la Roma, ambalo ni Kanisa la mashahidi.

Misa ya liturujia ya Ethiopia na Asmara

Kardinali Gugerotti, alisema kuwa Kanisa lao ni Kanisa tukufu ambalo mizizi yake ya Kikristo ilisitawi katika muktadha maalum, ulioangaziwa pia na mateso. "Ni kweli kwamba katika historia yao bado kuna nyakati za mateso makubwa, kutokana na vita, migawanyiko, kutokana na kiburi, lakini Kanisa hilo halina cha kudai isipokuwa haki ya kutenda mema." Kwa kusisitiza zaidi alisema kuwa "Mkristo hawezi kuishi bila upendo - hivyo basi aliotoa ombi la "kuweza kuitekeleza Ethiopia na Eritrea." Jubilei hii ni ishara ya matumaini, kwa sababu mahali ambapo mtu anasali, kama walivyofanya hapo, kuna Bwana na Mungu yupo, na maisha hustawi. Makanisa ya Kikatoliki ya Ethiopia na Eritrea yameundwa kisheria kama Makanisa makuu juu ya  Shiria kamili  ambayo  ni ya utamaduni wa  Aleksandria na yanafanana na liturujia ya ghe'ez kwa pamoja.

Mjini Roma kukiwa na, mapadre wa baadaye wa Kanisa la Ethiopia na Kanisa la Eritrea wanafunzwa katika Chuo cha Kipapa cha Ethiopia. Hali ya kiroho ya Makanisa haya ina mizizi ya kina kibiblia, kuanzia historia ya malkia wa Sheba, aliyevutwa na hekima ya Mfalme Sulemani, iliyosimuliwa katika Kitabu cha Wafalme (1 Wafalme 10) na Mambo ya Nyakati (2 Mambo ya Nyakati 9), na ya mwanawe Menelik, ambaye alikuja kuwa mrithi wa kiti cha Axum, hadi tukio la shemasi  Filipo lililosimuliwa na kitabu cha Matendo ya Mitume, kuhusiana na mkutano na afisa wa Malkia Candace.

Mavazi ya kipapa na Misa ya Ethiopia na Asmara
13 Mei 2025, 11:18