Tafuta

2025.01.01 Ufunguzi wa Mlango Mtakatifu Basilika ya Mtakatifu Maria Mkuu. 2025.01.01 Ufunguzi wa Mlango Mtakatifu Basilika ya Mtakatifu Maria Mkuu.  (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Jubilei,kufungwa kwa Milango Mitakatifu ya Basilika za Kipapa,kwanza ya Maria Mkuu

Ibada ya kuhitimisha Mwaka Mkatatifu kwa kufunga Milango mitakatifu itaaanzia katika Basilika ya Mtakatifu Maria Mkuu Desemba 25,Itafuata Basilika ya Mtakatifu Yohane Laterano Desemba 27 na Dominika tarehe 28 Desemba itakuwa Basilika ya Mtakatifu Paulo Nje ya Ukuta.

Vatican News

Mlango Mtakatifu wa Basilika ya Mtakatifu Maria Mkuu utakuwa wa kwanza kufungwa kati ya Basilika za kipapa wakati wa Jubilei ya 2025. Sherehe hiyo itafanyika Siku ya Noeli  saa 11:00 jioni na itaongozwa na Mkuu wa Basilika ya Liberia, Kardinali Rolandas Makrickas. Kufuatia hili, Jumamosi, Desemba 27, utafungwa  Mlango Mtakatifu wa Basilika ya Mtakatifu  Yohane, Lateran. Ibada imepangwa kufanyika saa 5:00 asubuhi na itaongozwa na Mkuu wa Kanisa hilo Kardinali Baldo Reina. Siku inayofuata, Dominika tarehe 28 Desemba 2025, Mkuu wa Basilika ya Mtakatifu Paulo Nje ya Kuta, Kardinali James Michael Harvey, ataongoza ibada kama hiyo ya kufunga Mlango Mtakatifu.

Sherehe za Kufunga Mlango Mtakatifu wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Maria Mkuu

Mlango Mtakatifu wa Basilika ya Liberia(Mtakatifu Maria Mkuu), uliofunguliwa tarehe 1 Januari  2025, umewakaribisha mahujaji na waamini zaidi ya milioni ishirini kupitia milango yake. Tarehe ya kufungwa haikuchaguliwa kwa bahati mbaya: Mtakatifu Maria Mkuu kiukweli, ni Basilika ya Noeli Takatifu, mlinzi wa masalio ya Kitanda Kitakatifu ambapo Mtoto Yesu akiwa mchanga alipumzishwa. Kwa hiyo Sherehe ya kufungwa kwa Mlango huo itaanza kwa nyimbo za Masifu ya jioni  ikifuatiwa saa 12:00 kufungwa kwa ibada ya Mlango Mtakatifu, ikiambatana na kupigwa kwa kengegele yenye jina Sperduta,ambayo ni ya kale ya Basilika. Ili kuruhusu maandalizi ya ibada, Basilika itafungwa kwa umma saa 9:00 alasiri kwa waamini. Kisha ufikiawaji  utaanza saa 10:00 jioni  na utaruhusiwa, kulingana na upatikanaji, tu kwa kushiriki katika sherehe zilizopangwa. Hizi pia zitatangazwa kwenye skrini kubwa zitakzowekwa kwenye Uwanja wa Kanisa hilo Kuu la Mtakatifu Maria Mkuu kwa ajili ya wale ambao watakuwa  nje.

Ibada katika Mtakatifu Yohane Lateran na Mtakatifu Paulo Nje ya Kuta

Wakati huo huo Ibada ya kufunga Mlango Mtakatifu wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Yohane Lateran itafuatiwa na Ibada ya Misa Takatifu ikiongozwa na kwaya ya Jimbo la  Roma, na mwalimu wake  Monsinyori Marco Frisina. Wakati wa Mwaka Mtakatifu, Mlango Mtakatifu wa Yohane Laterano ulivukwa  na waamini wa parokia nyingi za Roma: jumuiya za parokia, ama moja moja au zilizopangwa katika wilaya, kwa kiasi kikubwa zilichagua kusherehekea Jubilei yao katika Kanisa kuu la Roma. Wamini pia wataweza kuingia kwenye basilika kwa tiketi ya bure kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 4:00 asubuhi, masaa ya Ulaya. Mara tu Mlango Mtakatifu wa Basilika ya Papa ya Mtakatifu Paulo Nje ya Kuta utakapofungwa, wataweza kushiriki kwa uhuru bila tiketi.

18 Desemba 2025, 15:45