Tafuta

2026.06.26  Mkutano Mkuu Maalum wa Makardinali mji i Vatican. 2026.06.26 Mkutano Mkuu Maalum wa Makardinali mji i Vatican.  (@Vatican Media)

Mkutano Mkuu sehemu ya kwanza ilihitimishwa kwa ishara ya amani

Alasiri ya majadiliano katika Ukumbi wa Paulo VI kwa ajili ya Makardinali waliokuwepo.Kulikuwa na makubaliano makubwa kuhusu hitaji la kufanya kazi ili kujenga amani na"ustaarabu wa upendo,"ikiwa ni pamoja na kupitia lugha ya kusikiliza na kusamehe.Makundi mengi yalishiriki hitaji la kuvuka mantiki ya vita vya haki na badala yake kuzungumzia haki ya ulinzi sawa.Papa Leo XIV alizungumza mwanzoni mwa kikao na tena mwishoni,akiongoza sala ya kufunga.

Vatican News

Hali chungu nchini Venezuela na waathiriwa wengi wa tetemeko la ardhi ni masuala yaliyofungua kikao cha alasiri Ijumaa tarehe 26 Juni 2026 cha Mkutano Mkuu Maalum uliofanyika katika cha Ukumbi wa Paulo VI, mjini Vatican. Kikao kuhusu mada "Utamaduni wa Nguvu na Ustaarabu wa Upendo," kilichojitolea kutafakari Sura ya V ya Waraka wa Magnifica Humanitas, kilianza na sala ya pamoja na udhibiti wa Kardinali Pablo Virgilio Siongco David, ambaye kisha alimpatia  nafasi Kardinali Víctor Manuel Fernández, Mwenyekiti wa  Baraza la Kipapa la Mafundisho Tanzu ya Kanisa, kwa ajili ya hotuba yake ya utangulizi. Papa Leo XIV  alihudhuria kikao mwanzoni na akarudi tena kwa kikao cha jumla.

Kurekebisha vita na mgawanyiko

Kazi ilianza, huku vikundi 11 vikiripoti katika  Ukumbi, 8 kutoka kundi la kwanza pamoja na 3 kutoka kundi la pili. Kila mtu alizungumzia masuala muhimu ya wakati huu, "nguvu inayopunguza utu wa utamaduni wa madaraka," "umoja wake, jaribu la kufuata mantiki ya wenye nguvu, kurekebisha vita na mgawanyiko, ambavyo husababisha kupungua kwa kizingiti cha uvumilivu wa vurugu na kurahisisha hatari katika kutafuta suluhisho," kulingana na taarifa kutoka Ofisi ya Vyombo vya Habari ya Kiti Kitakatifu.   Kwa hivyo wito wa uwajibikaji katika kujenga amani na ustaarabu wa upendo, kwa ushuhuda wa kuaminika, kwanza kabisa ndani ya Kanisa, wa hitaji la lugha inayowajali watu, iliyotengenezwa kwa kusikiliza, msamaha, upatanisho, haki ya kurejesha, na ishara. Lugha inayoweza kugusa mioyo ya wale walio katika migogoro na inayoweza kuelewa majeraha yanayosababishwa na vita, "lugha inayowezesha utafutaji wa umoja katika Kanisa."


Wajibu wa Kujenga Amani Umoja ndani ya Kanisa kwa ajili ya uaminifu na mazungumzo muhimu na imani na dini zingine, hasa Uislamu: hili lilikuwa jambo lingine lililosisitizwa katika mijadala ya vikundi. "Katika wakati ambapo utandawazi wa kutojali unatufanya tusivumilie mateso ya wengine," kila mtu lazima achukue jukumu la kujenga amani. Kwa mtazamo huu, vikundi vyote vilisisitiza umuhimu wa imani katika Kristo, wa Injili inayobadilisha ulimwengu tunapokataa nadharia yake tu, na wa wito wa awali wa Kanisa, kwa sababu kuna hali zinazohitaji kuingilia kati kwa Mungu kushughulikiwa. Katika mtiririko huo, baadhi ya vikundi kisha viliakisi kazi ya Kanisa katika Nchi Takatifu na Ulaya Mashariki. Mjadala pia ulizungumzia jukumu la nguvu ya kisiasa, isiyo na uhusiano wake wa sumu na nguvu ya kiuchumi. Familia, elimu, ugumu wa kupita zaidi ya mantiki ya majibu ya papo hapo, na hitaji la uinjilishaji wa ujasiri pia vilijadiliwa. Vikundi mbalimbali vilitaja jukumu la diplomasia ya Kiti Kitakatifu na Wawakilishi katika kusikilizwa kwa sauti ya Kanisa.

Kusimama kando ya Papa katika wito wake wa amani

Katika muktadha huo, hitaji liliibuka la kuvuka mantiki ya vita vya haki, kwani Injili haiwezi kulazimishwa kwa nguvu, na kusema badala ya haki ya ulinzi sawa. Shukrani kubwa ilitolewa kwa Papa Leo XIV kwa ajili ya Waraka wake wa Kitume wa Magnifica Humanitas, kwa kulaani migogoro na wito wake wa amani. Pia kulikuwa na tafakari kuhusu munus Petrine, dhamana ya uhuru wa Kanisa kutoka katika mamlaka ya kisiasa, na hitaji la ishara ambazo zinaweza kuwa alama za amani katika wakati huu.


Wito wa Kuwajibika

Hatimaye, kulikuwa na wakati wa kuingilia kati kibinafsi kuhusu mada za kikao hicho. Baadhi ya makardinali walitoa shukrani kwa nafasi ya kushiriki iliyowakilishwa na Mkutano Mkuu huo pia wakisisitiza hitaji la kufanya kazi pamoja na viongozi wa dini zingine ili kuthibitisha ustaarabu wa upendo. Baadhi waliripoti majibu ya wengi kwa maneno makali ya Papa katika Ensiklika kuhusu kuchelewa kwa Kanisa kukemea utumwa; maneno yaliyofungua mioyo yao. Makardinali walisisitiza kwamba Waraka wa Papa  pia ni wito kwa Baraza la Makardinali kuchukua jukumu la kujenga amani, ikiwa ni pamoja na kupitia alama kama vile Mkutano wa Maombi kwa ajili ya Amani ulioitishwa na Mtakatifu Yohane  Paulo II huko Assisi mnamo 1986. Mwishoni mwa kikao, saa 1:30 jioni , Baba Mtakatifu  Leo  XIV aliongoza sala ya kufunga.


MKUTANO MKUU WA MAKARDINALI

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here.

 

27 Juni 2026, 09:37