Mashambulizi ya Bandari ya Sudan:mmisionari,awamu mpya ya vita inaanza!
Vatican news
Ikiwa mashirika ya kimataifa yatalazimika kuondoka eneo la Bahari Nyekundu, "mgogoro wa kibinadamu utakuwa mbaya zaidi."Kwa siku ya tatu mfululizo, mashambulizi ya ndege zisizo na rubani yanayohusishwa na jeshi la Sudan kwa Wanajeshi wa Msaada wa Haraka (RSF) yalilenga Bandari ya Sudan, kwenye Bahari Nyekundu. Katika mji huo, kitovu cha Sudan na mji mkuu wa muda baada ya kuzuka kwa mzozo huo, tangu tarehe 15 Aprili 2023, uwanja wa ndege na kituo cha kijeshi vilipigwa, na kusababisha moto mkubwa na nguzo za moshi, ambao pia ulipanda kutoka ghala kuu la mafuta la nchi hiyo ya Kiafrika.
"Hali inatia wasiwasi sana kwa sababu Bandari ya Sudan imekuwa kimbilio, "mahali salama" kwa maelfu ya watu ambao walikumbwa na ghasia za vita na ambao walilazimika kukimbia ardhi zao, lakini pia kwa mashirika ya kibinadamu, ambayo yamejikita hapa kufanya kazi na kuhudumia idadi ya watu", alishuhudia hayo Padre Jorge Naranjo, mkurugenzi wa chuo cha sayansi na teknolojia cha Comboni huko Bandarini Sudan. "Uwanja wa ndege wa kimataifa umekuwa ndio pekee unaofanya kazi nchini katika miezi hii na, baada ya shambulio la kwanza, usiku kati ya Jumamosi na Jumapili iliyopita, safari za ndege zilisimamishwa na kisha kurejeshwa alasiri, lakini jana usiku kulikuwa na shambulio jipya na kwa hivyo lilifungwa."
Kama tahadhari, Shirika la Umoja wa Mataifa la Huduma ya Kibinadamu ya Anga (UNHAS) limesitisha kwa muda safari za ndege kwenda na kutoka jijini. Picha ambayo inazidisha mzozo mkubwa zaidi wa kibinadamu duniani, kama Umoja wa Mataifa ulivyofafanua hali ya Sudan, yenye karibu watu milioni 13 waliokimbia makazi na zaidi ya wakimbizi milioni 3 ambao wamekimbilia nchi jirani.
Katika Bandari ya Sudan, "hakujakuwa na umeme kwa zaidi ya majuma mawili kwa sababu mtambo wa kufua umeme wa Meroë, ambapo bwawa katika Mto Nile lilisimama, na transfoma ambazo zilisambaza umeme kwa nchi nzima ziliathirika." Kwa mujibu wa mmisionari wa Comboni wa Hispania, aliongeza kkuwa “ Kwa sasa nchini Sudan tangu 2008, "hata bohari za gesi na petroli zimelengwa, jambo ambalo linapendekeza kwamba hizo zitakosekana hivi karibuni pamoja na umeme."
Jeshi chini ya uongozi wa Jenerali Abdel Fattah al-Burhan, ambaye hivi karibuni aliuteka tena mji mkuu Khartoum, kwa hakika lilikuwa limeimarisha udhibiti wake kaskazini na mashariki mwa nchi hiyo katika zaidi ya miaka miwili ya vita, huku wanamgambo wa Jenerali Mohamed Hamdan Dagalo wakiwa zaidi katika eneo la magharibi la Darfur na katika baadhi ya maeneo ya kusini.
Sasa, hata hivyo, "awamu mpya ya vita hivi" inaanza, alisema Padre Jorge, akiripoti ujenzi upya uliotolewa na jeshi. "Vikosi vya Msaada wa Haraka vimepokea ndege zisizo na rubani za hali ya juu zaidi za kiteknolojia zenye uwezo wa kusafiri umbali mrefu, ambayo inaonyesha mashambulio ya mbali. Kulingana na msemaji wa jeshi, inaonekana kwamba mashambulizi hayo yalitoka mashariki, kutoka kambi ya Bosaso, nchini Somalia, hata kama awali baadhi walikuwa wamezungumza kuhusu uvamizi kuanzia kusini mwa Libya."