Tafuta

Eneo la tukio la mfyatuaji risasi aliyeripotiwa katika Kituo cha Kiislamu huko San Diego,nchini Marekani. Eneo la tukio la mfyatuaji risasi aliyeripotiwa katika Kituo cha Kiislamu huko San Diego,nchini Marekani.  (REUTERS)

Marekani,Shambulio la Msikiti wa San Diego:Watu 5 wafariki

Kituo cha Kiislamu cha Marekani kilishambuliwa na watu wenye bunduki na kusababisha vifo vya watu watatu,pamoja na washambuliaji wawili walioripotiwa kujiua.Polisi wanachunguza nia ya mauaji hayo,lakini kwa sasa nadharia inayowezekana zaidi ni "uhalifu wa chuki."New York inaimarisha usalama katika misikiti yote jijini.

Na Paola Simonetti - Vatican.

Kengele ililia muda mfupi baada ya saa sita mchana, saa za San Diego, nchini Marekani tarehe 18 Mei 2026. Polisi walifika katika msikiti wa eneo hilo ambapo waliwakuta waathiriwa watatu waliokufa kwa risasi, akiwemo mlinzi Baba wa watoto nane kwa mujibu wa mke wake na  ambaye, kulingana na maafisa, alikuwa na jukumu muhimu katika kuzuia janga kubwa zaidi. Ndani ya dakika chache, tahadhari nyingine zilitolewa kwa milio mipya ya risasi iliyokuwa  umbali wa vitalu vichache, kwa bahati nzuri bila majeruhi zaidi. Washambuliaji wawili kisha walijifungia kwenye gari ambapo walipatikana wamekufa kutokana na majeraha ya kujidhuru. Imeripotiwa kwamba jumbe zenye madai ya "kiburi cha ubaguzi," bunduki hiyo ilikuwa na kauli mbiu "hotuba ya chuki," na kopo la petroli lenye stika ya SS chini.

Sababu ya shambulio

Uchunguzi kuhusu mauaji hayo unaendelea, lakini vyombo vya sheria vinazingatia hali ya "uhalifu wa chuki", kutokana na mvutano unaozunguka Mashariki ya Kati yenye misukosuko, ambayo pia ilishuhudia shambulio jingine kwenye sinagogi huko Michigan Machi iliyopita. Kulingana na picha zilizotolewa, operesheni hiyo katika saa chache zilizopita ilishuhudia mwitikio mkubwa wa vyombo vya sheria, huku maafisa wapatao mia moja wakishika doria katika eneo la msikiti baada ya ufyatuaji risasi. Hii ilikuwa siku tulivu kiasi, bila umati wa sala za Ijumaa. Shule ya karibu ya Al Rashid pia ililindwa, huku watoto wote waliokuwa ndani ya jengo hilo wakiondolewa mara moja.

Maoni 

Imam Taha Hassane wa Kituo cha Kiislamu cha San Diego, akitoa wito wa uvumilivu wa kidini, alisema kwamba "jumuiya nzima inaomboleza. Ni jambo ambalo hatukutarajia," aliongeza katika mkutano na waandishi wa habari, "lakini wakati huo huo, kutovumiliana kidini na chuki ambazo kwa bahati mbaya zipo katika taifa letu hazijawahi kutokea." Akifahamishwa kuhusu tukio hilo, Rais wa Marekani Donald Trump anafuatilia matukio. Meya wa Los Angeles Karen Bass alionesha hasira yake kuhusu ufyatuaji risasi: "Mahali pa ibada," alisema, "panapaswa kuwa mahali patakatifu, ambapo chuki na vurugu hazina nafasi." Jiji la New York linafunga misikiti yake, kufuatia agizo kutoka kwa Meya Zohran Mamdani la kuimarisha hatua za usalama kama tahadhari, ingawa hakujawa na vitisho hadi sasa.

Imesasishwa tarehe 19 Mei 2026 saa 8.00 na Angella Rwezaula - Vatican.

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here.

19 Mei 2026, 13:43