UN:Alaani uamuzi wa kusimamisha uchaguzi nchini Nicaragua
Vatican News
Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, alilaani ukandamizaji mpya dhidi ya haki za kiraia na kisiasa nchini Nicaragua, kufuatia tangazo la Rais Daniel Ortega kwamba atasimamisha kufanyika kwa uchaguzi mpya, na kutoa wito kwa mamlaka ya Nicaragua kufungua tena nafasi ya kiraia na kurejesha utawala wa sheria.
Bunge:Kubadilisha uamuzi wa Ortega kuwa Sheria
Spika wa Bunge la Nicaragua Gustavo Porras alitangaza kwamba Bunge litawasilisha mageuzi ifikapo mwisho wa Julai ili kugeuza maamuzi ya Ortega kuwa sheria. Kulingana na Porras, hatua hiyo itatumika kupinga kuingiliwa na wageni na kulinda kile alichokiita "demokrasia ya watu wa Nicaragua," akisema kwamba raia wa nchi hiyo wataamua "lini na vipi" uchaguzi wowote utafanyika.
Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here.