Tafuta

2025.11.20 Papa akiwa na Jumuiya ya Wamonaki wa kiagostinian. 2025.11.20 Papa akiwa na Jumuiya ya Wamonaki wa kiagostinian.  (@Vatican Media)

Papa atembelea wamonaki wa kiagostinian:"ni mtu mwenye utulivu"

Ilikuwa ni wakati mzuri kukaa na watawa wa familia ya Mtakatifu Agostino kama Yeye ambao Papa Leo XIV alichagua kuwa kituo cha pili cha ziara yake fupi kwenda Umbria,mara baada ya kwenda Assisi kukutana na Baraza la Maaskofu Italia,ambao walihitimisha Mkutano wao Mkuu wa 81,Novemba 20."Ulikuwa ni wakati wa kufahamiana zaidi na mtu tuliyemjua kwa miaka mingi."Alisema hayo Mkuu wa Monasteri Sr Maria Cristina Daguati wakati wa kutoa maoni kwa vyombo vya habari vya Vatican.

Na Tiziana Campisi – Vatican.

Baada ya kukutana na Maaskofu wa Italia huko Assisi, Baba Mtakatifu Leo XIV Alhamisi tarehe 20Novemba 2025 alitembelea Jumuiya ya watawa wa Monasteri ya Kiagostinian, ya Mtakatifu Clara huko Montefalco kwa ziara ya kibinafsi. Monasteri hiyo inajulikana kwa kuhifadhi kumbukumbu ya Mtakatifu Clara, inayojulikana kama Conventi ya Msalaba. Papa alitumia muda wake kukaa na watawa, kisha akaadhimisha ibada ya Misa na hatimaye akala chakula cha mchana nao. Hata hivyo Papa aliwahi kwenda huko kama Padre, kisha katika matukio mengine akiwa  Mkuu wa Shirika la  Mtakatifu Agostino, na kwa njia hiyo amerudia akiwa kama  Baba Mtakatifu wa 267 wa Kanisa la Ulimwengu.

Ndani ya Monasteri ya Mtakatifu Clara
Ndani ya Monasteri ya Mtakatifu Clara   (@Vatican Media)

Kwa hiyo ziara hii ilikuwa ni wakati wa ushirika na watawa wa familia ya Kiagostinian waliovalia sare, ambao Papa Leo XIV alichagua kama kituo cha pili katika ziara yake fupi  ya Umbria, baada ya kwenda Assisi kukutana na Baraza la Maaskofu Italia(CEI), ambao walihitimisha Mkutano wao Mkuu wa 81.


Kwa upande wa  Mkuu wa Monasteri  Sr Maria Cristina Daguati alitoa maoni kwa vyombo vya habari vya Vatican kuwa, "Wakati wa kufahamiana zaidi na mtu tunayemjua kwa miaka mingi. Papa Leo XIV ameleta mazingira mazuri ya maombi. Kwa hivyo sio kwamba alitusumbua sana, ilikuwa vizuri sana. Nzuri... "Ni urafiki mzuri, kwa sababu ni wazi tumemjua kwa miaka mingi, na kwa hivyo ningesema kila kitu kilijitokeza katika roho ya kufahamiana sana," aliongeza Sr Daguati "siku rahisi sana" na "mtu mwenye "utulivu."

Papa alitembelea Watawa wa kiagostinian huko Montefalco

Makabirisho huko Montefalco

Papa Leo XIV hata hivyo aliondoka huko Assisi yapata saa 4:00 asubuhi masaa ya Ulaya. Alikuwa amefika kwa helikopta yapata saa 2:30 asubuhi kutoka mjini Vatican  katika Uwanja wa Migaghelli, kisha aakaenda katika Basilika ya Mtakatifu Francis na akakaa kimya kwa maombi mbele ya kaburi la Mtakatifu Francis. Baada ya hapo alihamia katika Basilika ya Mtakatifu Maria wa Malaika (Maria degli Angeli,) ambapo alizungumza na Maaskofu wa Baraza la Maaskofu Italia (CEI), kabla ya kwenda na helikopta huko Montefalco.


Katika mji huu mdogo katika jimbo la Perugia, kulikuwa na msisimko mkubwa kuhusu kuwasili kwa Papa Leo XIV, Papa wa kwanza kutembelea maeneo hayo. Meya wa mji Alfredo Gentili na Naibu Meya Daniele Morici walimkaribisha kwenye uwanja wa michezo.

Picha ya pamoja ya jumuiya
Picha ya pamoja ya jumuiya   (@Vatican Media)

Watu wengi walikusanyika kando ya mitaa ya kale kati kumlaki. Watoto kadhaa walimsubiri kwa furaha karibu na monasteri, na Papa aliwapungia mkono kutoka kwenye gari lake kabla ya kuingia katika monasteri ya kale ya Mtakatifu Clara  ambayo asili yake inaanzia katika karne ya 13.

L'arrivo del Papa a Montefalco

Baada ya kufika Papa huko Montefalco (@Vatican Media)

Jumuiya ya Wamonaki na watawa wa Mtakatifu Clara wa Montefalco

Katika jumuiya ya watawa ambayo inafuata Kanuni ya Mtakatifu Agostino tangu tarehe 20 Juni 1290, na ambayo leo hii ina watawa 13, ushuhuda wa Clara wa Montefalco unaendelea. Huyu ni Mtawa wa Kiitaliano aliyezaliwa mwaka 1268 na kufariki mwaka 1308. Sura yake  inahusishwa na Montefalco ambapo pia ni kijiji cha Umbria kinachojulikana kwa mandhari yake, harufu, na ladha, na pia kwa uzalishaji wake wa divai, kama vile 'Sagrantino di Montefalco.' Alikuwa mtawa aliyetangazwa kuwa Mtakatifu mwaka 1881 na Papa Leo XIII. 

Papa na watawa wa kiagostinian
Papa na watawa wa kiagostinian   (@Vatican Media)

Katika maisha yake alikuwa na umri wa miaka sita alipoonesha hamu ya kujitoa kwa Mungu na kufanya toba, kama dada yake Giovanna akiwa na umri wa miaka sita. Akiwa aliyachiliwa akiwa na umri wa miaka ishirini na mitatu tu, alitoa msukumo mpya kwa Jumuiya ya Kitawa, akipanga maisha ya pamoja vizuri zaidi, akiwataka masista wote kufanya kazi za mikono, lakini akiwapa uhuru wa kutosha wale waliopenda zaidi kusali. Alijitambulisha kama mwanamke mwenye uthabiti ulioelimika. Watu wengi maskini na wenye uhitaji walimkaribia, na Clara alikuwa tayari kila wakati kuwapa chakula au neno la faraja.

Mtakatifu Clara wa Montefalco

Kwa wanaume waliosoma, makuhani, na mapadre  wa juu, alikuwa mshauri mwenye busara, mwenye uwezo wa kusoma mioyo ya wengine na kuona matukio. Yote haya licha ya jaribio kali la ukame wa kiroho ulimsumbua kwa miaka 11. "Nina Yesu wangu moyoni mwangu," alirudia baada ya Kristo kumtokea katika bustani ya monasteri kama msafiri anayeteseka, akimwambia: "Natafuta mahali pazuri ambapo naweza kupanda Msalaba, na hapa ndipo ninapopata mahali pazuri." Simumuli inasema kwamba Yesu, kama msafiri, alimpatia fimbo yake, na kwamba ilipopandwa, ilizaa mti, ambao bado unastawi hadi leo hii .

Papa akisalimiana na Meya wa Mji
Papa akisalimiana na Meya wa Mji   (@Vatican Media)

Ni Melia Azedarach, asili ya Himalaya, au "mti wa Mtakatifu Clara," ambao mbegu zake za miti zimetumika kwa karne nyingi kutengeneza rozari. Clara alifariki mnamo tarehe 17 Agosti  1308, na watawa wenzake waliamua kuhifadhi mwili wake. Kwa sababu hiyo, viungo vyake viliondolewa, na ishara za Mateso ya Kristo ziligunduliwa moyoni mwake: "katika umbo la mishipa migumu ya nyama, upande mmoja msalaba, misumari mitatu, sifongo, na mwanzi; na upande mwingine nguzo, mjeledi... na taji...

Wakati wa misa
Wakati wa misa   (@Vatican Media)

Katika mfuko wa nyongo... kulipatikana mawe matatu ya mviringo, yote yanafanana... ambayo yanawezekana yaliwakilisha Utatu." Sifa ya Clara ya utakatifu ilienea haraka, na miujiza kadhaa kupitia maombezi yake iliandikwa. Alitangazwa kuwa Mtakatifu na Papa Leo XIII mnamo tarehe 8 Desemba 1881.

Kaburi la Mtakatifu Clara
Kaburi la Mtakatifu Clara   (@Vatican Media)

Misa ya Papa katika Kanisa la Mtakatifu Clara

Papa alitumia muda kuzungumza na watawa hawa, kisha akaadhimisha Misa katika Kanisa zuri la karne ya 17 lililobuniwa na mbunifu wa Peru, Valentino Martelli. Katika sehemu ya kulia, nyuma ya reli, kuna chombo cha fedha chenye mabaki ya Mtakatifu Clara. Madhabahu iliyowekwa wakfu kwake ina sehemu kubwa ya mbele ya stucco, iliyopambwa kwa nguzo, mahindi, fremu za mapambo, na sanamu mbili katika sehemu mbili za pembeni, zinazowakilisha Watakatifu Agostino na Jerome.

Wakati wa misa
Wakati wa misa   (@Vatican Media)
Wakati wa misa ya Papa na wamonaki wa kiagostinian
Wakati wa misa ya Papa na wamonaki wa kiagostinian   (@Vatican Media)

Sehemu zingine mbili zilizofunikwa na reli zina mabaki zaidi ya Clara, ikiwa ni pamoja na moyo wake, Siri za Mateso ya Kristo zilizogunduliwa hapo msalabani, na mawe matatu yaliyopatikana kwenye kibofu chake cha nyongo. Lakini mahali pa kusisimua zaidi pa Clara ni Kanisa la Msalaba Mtakatifu, lililopambwa kwa michoro mizuri ya karne ya 14. Hapo awali, Kanisa dogo alilokuwa amejenga na mahali palipochaguliwa kwa siku zake za mwisho za maisha yake, inasemekana kwamba miujiza mingi iliyosimuliwa katika michakato ya kutangazwa watakatifu ilitokea hapo.

Leone XIV a pranzo con le monache agostiniane

Paa Leo XIV amekula chakula na watawa wa ndani wa kiagostino(@Vatican Media)

Chakula cha Mchana na Watawa

Watawa walimpatia  Papa chakula cha mchana cha kawaida cha Umbria. Mkuu wa Monasteri Cristina Daguati, na watawa wenzake waliwasilisha kalenda ya 2026, "Kuelekea Amani Isiyo na Silaha," pamoja na maandishi kutoka katika hotuba na mahubiri yake na ya Mtakatifu Agostino, na michoro ya Sr Maria Rosa Guerrini, Mkuu mpya aliyechaguliwa hivi karibuni wa Shirikisho la Watawa wa Kiagostino nchini Italia, Picha ya Bikira Maria Mama wa Ushauri Jema " shirikisho alilokutana nalo hivi karibuni tarehe Novemba 12.

Papa na watawa waaagostinian
Papa na watawa waaagostinian   (@Vatican Media)

Asante kwa kusoma makala haya. Ikiwa unataka kuendelea kupata taarifa mpya, tunakualika ujiandikishe kwa jarida letu hapa: cliccando qui

20 Novemba 2025, 17:17