Ziara ya 4 ya Kitume ya Papa Leo XIV:Sasa yuko nchini Hispania

Hatimaye ziara ya Kitume iliyotamaniwa sasa imefika.Baba Mtakatifu Leo XIV yuko nchini Hispania kuanzia Juni 6 -12,2026. Amepokelewa na wenyeji wake kwa shangwe kuu.

Vatican News

Asubuhi ya Jumamosi, tarehe 6 Juni 2026, saa 10:12 asubuhi kwa saa za huko, Papa Leo XIV aliwasili nchini Hispania. Baada ya safari ya ndege ya takriban saa mbili na nusu, Shirika la "Ndege ya ITA Airways A320" ilitua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Adolfo Suárez Madrid-Barajas, ambapo makaribisho rasmi yalifanyika. Huu ni mwanzo wa Ziara yake ya nne ya kitume ya kimataifa ya Baba Mtakatifu nchini Hispania hadi Juni 12.

Mara baada ya kutua kwa Ndege, Papa alitoka nje
Mara baada ya kutua kwa Ndege, Papa alitoka nje   (@Vatican Media)
Papa alifika na kupokelea na familia ya kifalme nchini Hispania
Papa alifika na kupokelea na familia ya kifalme nchini Hispania   (@Vatican Media)
Papa akikagua Gwaride akiwa na mwenyeji wake
Papa akikagua Gwaride akiwa na mwenyeji wake   (@Vatican Media)

Padre Josep Maria Turull, Msimamizi wa Kanisa Kuu la Familia Takatifu Barcelona alielezea katika mahojiano na vyombo vya habari vya Vatican wakati wanamsubiri Papa Leo, kwamba, kuhusiana na Basilika hiyo ambayo Papa atatembelea anaweza kufichua kwa sehemu ya maelezo machache ya ziara ya Askofu wa Roma. Anazungumza na utulivu wa subira wa mtu anayejua kwamba mambo makubwa huchukua muda. Utulivu unaowafaa wale wanaotunza mahali ambapo, tayari kuna zaidi ya miaka 140, bado haujakamilika. Baada ya yote, kama Gaudí mwenyewe, ambaye mchakato wake wa kutangazwa kuwa mtakatifu unaendelea na ambaye ametangaza kazi yake kuwa "kazi ya Mungu kuwa," alisema, "mteja wangu hana haraka."

Huko Hispania, Papa atakutana na urithi tajiri wa kihistoria na kiutamaduni huku akikutana na wawakilishi wa Kanisa na taasisi za umma, pamoja na maelfu ya vijana, familia, na watu mashuhuri kutoka ulimwengu wa michezo, utamaduni, na burudani baadhi yao watashiriki katika matukio ya umma. Mazungumzo kati ya Kanisa, siasa na utamaduni kama zana za kushinda mgawanyiko, pamoja na kutafakari maendeleo ya kiteknolojia na kibinadamu pia kwa kuzingatia Waraka wa Magnifica Humanitas wa hivi karibuni, yatakuwa miongoni mwa mada kuu za hotuba, salamu, na hotuba 23 za Papa.

Papa Leo XIV akiwa Hispania ataona hali halisi ya Nchi hiyo. Kwa hivyo fundisho la Antoni Gaudí ni la wakati muafaka sana, hasa kwa wakati wetu na kwa Ulaya, ambapo uenezaji wa imani ndani ya familia umekatizwa kwa ufanisi na ambapo uinjilishaji wa kwanza hauwezi kuchukuliwa kirahisi. Hatimaye, kituo huko Kisiwa kikubwa cha Kanari na Tenerife kinatoa uzoefu wa moja kwa moja wa hali ngumu ya wahamiaji. Wakipona kwa kuvuka, wanagonga milango ya Ulaya, ingawa bara hilo mara nyingi hushindwa kushughulikia dharura hii kwa njia iliyoratibiwa na kupangwa, na kuziacha nchi zilizo hatarini zaidi, ikiwa ni pamoja na Hispania pekee yake.

Dominika tarehe 7 Juni 2026  Papa Leo XIV ataadhimisha Sherehe za Mwili na Damu ya Yesu na kwaya ya Monasteri ya Mtakatifu Lorenzo de El Escorial, itashiriki ikileta sauti ya moja ya jumuiya za kidini zenye uwakilishi mkubwa nchini katika mji mkuu huo wa Madrid.

Papa nchini Hispania
Papa nchini Hispania

Injili inatangazwaje leo hii katika muktadha wa jamii iliyo na alama kubwa ya tamaduni  kubwa ya Kikristo ambayo imeunda utambulisho wake, lakini ambayo leo hii inaonekana kuwa ya kidunia zaidi? Hili ndilo swali litakaloenea katika hija nzima ya Askofu wa Roma Huko Barcelona, ​​​​hasa wakati wa ziara yake kwenye Basilika  kubwa ya Familia Takatifu(La Sagrada Familia), ambapo Papa atazindua mnara mrefu zaidi uliowekwa wakfu kwa Yesu Kristo, jibu linalowezekana liko: kupitia lugha ya uzuri. Kanisa limekuwa likizungumza na kila mtu kupitia sanaa, na hasa kupitia picha.

Asante kwa kusoma makala yetu. Unaweza kuendelea kupata habari mpya kwa kujisajili kwa jarida letu la kila siku: Just click here.

06 Juni 2026, 13:41